• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Mipango
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Mkurugenzi wa Afya TAMISEMI asema vituo vya Afya Kifanya na Makowo ni miradi ya kuigwa

Tarehe iliyowekwa: February 19th, 2021

Mkurugenzi wa Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Ofisi ya Rais-TAMISEMI Dr.Ntuli Kapologwe amepongeza kasi ya ujenzi wa vituo vya afya unaofanywa na Halmashauri ya Mji Njombe ambapo mpaka sasa Halmashauri ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha vituo viwili vya Afya Makowo na Kifanya kupitia michango ya Wananchi na mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo.

Akizungumza wakati wa ziara yake ambapo alipata nafasi ya kutembela Kituo cha afya Kifanya Dkt Ntuli amesema kuwa Halmashauri ya Mji Njombe ni miongoni mwa Halmashauri zilizoweza kufanya vizuri kwenye utekelezaji wa miradi ya afya kupitia mapato ya ndani na ni vyema Halmashauri nyingine kuiga mfano huo.

“Uongozi unaweza kufanya mabadiliko makubwa sana. Menejimenti mnaongea lugha moja hicho ni kitu kizuri sana na ndio maana kwa pamoja mnaweza kutekeleza haya yote. Hayo maono uliyonayo na dhana ya ushirikishwaji na mikakati ni mambo ambayo Wakurugenzi katika maeneo mengine wanatakiwa waige mfano kama huu. Kuna maeneo mengine Wakurugenzi hata kushiriki katika kutekeleza miradi ya afya ni ngumu. Nimefurahi kwani kwa kipindi nilipokuja mathalani katika Hospitali ya Kibena na leo nilivyoiona mabadiliko ni makubwa sana niwapongeze sana.Lakini kubwa kwenye vituo vya afya mmepiga hatua kubwa”Alisema Dr. Ntuli

Dr. Ntuli amesema kuwa ni vyema katika Vituo vya Afya kuweka uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti ya matunda kwenye bustani zinazozunguka maeneo ya Hospitali 

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda amesema kuwa Halmashauri imejiwekea utaratibu wa kufanya vikao viwili kila wiki ambapo menejimenti hujadili taarifa za mapato katika vyanzo vyote zikiwemo hospitali na vituo vya afya  jambo ambalo Wakuu wa Idara hushiriki na kutoa mawazo juu ya jitihada za ukusanyaji mapato.

“Kwenye makusanyo huwa tunakusanya kwa asilimia mia moja na  kuwa na zidio.Hii imepelekea Halmashauri kuweza kupeleka fedha katika miradi  ya afya na ndio maana kwa sasa tupo katika kukamilisha vituo viwili vya afya Kifanya na Makowo. Halmashauri kupitia mapato ya ndani zidio la makusanyo kwenye bajeti ya mwaka 2019/2020 kwa kituo afya Kifanya kilipokea milioni 290 na Makowo 290 milioni. Kuchangia jitihada za wananchi. Hiyo ikiwa ni kwenye zidio la makusanyo.” Alisema Mwenda.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Njombe Dr. Yesaya Mwasubila amesema kuwa changamoto kubwa kwa sasa mara baada ya kukamilika kwa vituo hivyo ni uwepo wa Madakatari na wataalamu wa mionzi ambapo Dr. Ntuli amesema kuwa Serikali imeendelea kulifanyia kazi jambo hilo kwa kuajiri Wataalamu katika Sekta hiyo.

Katika ziara hiyo Dr. Ntuli ameahidi upatikanaji wa vifaa tiba katika Vituo hivyo mara baada ya kukamilika na kuahidi uboreshaji wa kituo cha afya Njombe Mjini na ujenzi wa kituo kipya cha afya Mjimwema huku Halmashauri ikitaraji kuanzisha ujenzi wa kituo kingine kipya katika Kata ya  Luponde.

Matangazo

  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021,SHULE ZA KITAIFA, TEULE NA KUTWA WANAFUNZI WA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE December 18, 2020
  • FOMU ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021, SHULE ZA SEKONDARI KATIKA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE December 15, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA September 21, 2020
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Kudumu Bunge inayoshughulikia UKIMWI yafanya ziara Njombe

    March 02, 2021
  • Dugange Aipongeza Halmashauri ya Mji Njombe ujenzi wa Miradi ya Afya na Utoaji Asilimia 10 ya Mikopo

    March 01, 2021
  • Baraza la Waheshimiwa Madiwani Halmashauri ya Mji Njombe lapitisha rasimu ya bajeti 2021/2022

    February 26, 2021
  • Naibu Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi ateta na Watumishi Ardhi Mkoa wa Njombe-Awataka kufanya kazi kwa uzalendo

    February 25, 2021
  • Angalia zote

Video

Makala ya utekelezaji miradi ya maendeleo 2020 Halmashauri ya Mji Njombe
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe