• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

ASILIMIA 100 WAFAULU KIDATO CHA SITA – MIUNDOMBINU WEZESHI NA MOTISHA YATAJWA KUWA CHACHU YA MAFANIKIO

Tarehe iliyowekwa: July 9th, 2025

Na: Ichikael Malisa 

Kwa miaka miwili mfululizo (2024 na 2025), Halmashauri ya Mji Njombe imeendelea kung’ara kitaaluma baada ya wanafunzi wa kidato cha sita kutoka shule za sekondari za serikali kufanikisha ufaulu wa asilimia 100 kwa kupata daraja la kwanza hadi la tatu, ikiwa ni ongezeko kutoka asilimia 99.7 iliyorekodiwa mwaka 2021.

Akitoa tathmini ya matokeo ya mtihani wa kidato cha sita mwaka 2025, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Mji Njombe, Bw. Prochesius Mguli amesema mafanikio hayo yametokana na utekelezaji wa mpango kazi wa pamoja kati ya shule na Halmashauri, unaolenga kuinua kiwango cha ufaulu kwenye mitihani ya kitaifa.

Bw. Mguli ameongeza kuwa, mchango mkubwa umetolewa na Serikali kupitia maboresho ya miundombinu ya elimu, ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa, mabweni, mabwalo ya chakula, maabara za sayansi pamoja na upatikanaji wa huduma muhimu kama maji safi na umeme. Mazingira haya bora yameongeza utulivu na umakini wa wanafunzi katika masomo yao.

"Mazingira rafiki ya kujifunzia ni msingi wa mafanikio haya. Kwa mfano, Shule ya Sekondari Njombe imefanyiwa ukarabati mkubwa wa mabweni, bwalo na jiko; Yakobi Sekondari imejengewa mabweni manne ya wasichana, na Matola Sekondari imeongezewa mabweni manne pamoja na madarasa yaliyowezesha kuongezwa kwa mikondo mitatu mwaka 2025," alisema Bw. Mguli.

Ameeleza kuwa, ili kuendeleza hamasa na ushindani chanya baina ya shule, Halmashauri huwatunuku vyeti vya pongezi, zawadi na hata safari za kutalii kwa shule na walimu wanaofanya vizuri. Mfumo huu umejikita katika kutambua mchango wa kila mhusika kuanzia waalimu hadi watumishi wa kawaida.

"Menejimenti za shule zimeweka motisha ya fedha na zawadi kwa walimu na watumishi wote kuanzia kwa waalimu hadi wapishi  kwani kila mmoja ana nafasi kwenye matokeo. Mwaka jana, shule ya Sekondari Uwemba na Njombe zilipata fursa ya kutembelea Hifadhi ya Ngorongoro kama sehemu ya kutambua juhudi zao," aliongeza.

Ushirikiano mzuri kati ya walimu, wazazi, wanafunzi na viongozi wa serikali umeendelea kuwa sehemu muhimu ya mafanikio haya ya kitaaluma. Kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Halmashauri ya Mji Njombe imepokea zaidi ya shilingi bilioni 1.4, fedha zilizotumika kujenga shule mpya, madarasa, matundu ya vyoo, mabweni na kuboresha miundombinu ya shule za sekondari.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ASILIMIA 100 WAFAULU KIDATO CHA SITA – MIUNDOMBINU WEZESHI NA MOTISHA YATAJWA KUWA CHACHU YA MAFANIKIO

    July 09, 2025
  • WATENDAJI WA VIJIJI NA MITAA WAPEWA MAFUNZO YA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI.

    July 05, 2025
  • RUZUKU YA CHANJO YA MIFUGO,KINGA KWA MAENDELEO YA MIFUGO

    July 05, 2025
  • Dkt. Mhede azindua zoezi la chanjo ya ruzuku kwa mifugo Halmashauri ya Mji Njombe, dozi 227,000 kutolewa kwa ng'ombe na kuku

    July 05, 2025
  • Angalia zote

Video

ZIFAHAMU FAIDA ZA HERENI YA KIELEKTRONIKI KWA NG'OMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe