Baraza la Waheshimiwa Madiwani Halmashauri ya Mji Njombe Leo limepitisha rasimu ya bajeti ya kukusanya jumla ya Shilingi Bilioni 41.39 kwa mwaka 2022/2023,kati yake mapato ya ndani halisi ikiwa ni Shilingi Bilioni 5.17.
Akizungumza wakati wa kuwasilisha rasimu hiyo,Afisa Mipango wa Halmashauri ya Mji Njombe Shigela Ganja amesema kuwa katika makusanyo ya mapato ya ndani,fedha zitakazotumiwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni Shilingi Bilioni 3.1
Wakitoa mapendekezo yao katika rasimu hiyo baadhi ya Madiwani wamepongeza hatua hiyo lakini pia wametoa ushauri Mbalimbali ili bajeti hiyo iweze kuakisi matamanio ya Wananchi na kendelea kutoa mafanikio tarajiwa.
Kwa upande wake Mheshimiwa Edwin Mwanzinga Diwani wa Kata ya Matola ameshauri kuwa ni vyema Halmashauri ifanye upembuzi yakinifu wa vyanzo vya mapato ambavyo vimasimamiwa na Halmashauri yenyewe ambapo awali vilikuwa vya wazabuni.
"Tulikua na chanzo Cha ushuru wa choo lakini Kwa sasa tunakiendesha wenyewe naomba Wataalamu ifanyike tathmini ili kuona gharama za uendeshaji na salio linalobaki ili kuona kama faida ipo maana kwa jinsi ninavyoona inawezekana gharama za uendeshaji choo ziakawa kubwa ukilinganisha na kipindi ambapo tulikuwa na mzabuni."Alisema Mwanzinga
Kwa upande wake Mheshimiwa Ultrick Msemwa Diwani wa Kata ya Luponde ameshauri ni vyema zoezi la Ujenzi wa miradi ukazingatia kuanza mradi na kukamilisha wote ili kuepuka utawanywaji wa fedha katika miradi mingi ambayo kwa namna Moja miradi hiyo inachukua muda mrefu kukamilika kutokana na wingi wa miradi na upungufu wa fedha zinazotolewa.
Baraza la Madiwani Halmashauri ya Mji Njombe kwa pamoja limeridhia na kupitisha rasimu ya bajeti kwa mwaka 2022/2023.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe