• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

MAAMBUKIZI YA VVU TOKA KWA MAMA KWENDA KWA MTOTO YAFANIKIWA KWA ASILIMIA 99.5

Tarehe iliyowekwa: December 1st, 2022

Kila Disemba Mosi ya Kila Mwaka Dunia huadhimisha siku ya UKIMWI Duniani ambapo leo Katika Halmashauri ya Mji Njombe Maadhimisho hayo yenye Kauli Mbiu “Imarisha Usawa” ambapo Takwimu zinaonyesha kuwa Mkakati wa kuzuia Virusi vya UKIMWI toka kwa Mama kwenda kwa Mtoto umeweza kuwakinga Watoto wasipatwe na Maambukizi ya VVU kwa asilimi 99.5

Daniel Mwasongwe Mratibu UKIMWI Halmashauri ya Mji Njombe akisoma taarifa ya Kinga ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI toka kwa Mama kwenda kwa Mtoto kwa kipindi cha  Januari hadi Juni 2022 Jumla ya Wajawazito  150 walikuwa tayari wanaishi na maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI na Wajawazito 2727 waliweza kupima Virusi vya UKIMWI Ambapo  Kati yao 78 Walikutwa na Maambukizi ya VVU sawa na asilimia 2.9

Aidha, Kwa upande wa Wanaume 2058 waliohudhuria Kliniki ya Wajawazito kufanya huduma ya Upimaji VVU sawa na asilimia 75.5 ya Wanaume walitakiwa kuhudhuria Kliniki ambapo kati yao Wanaume 31 walikutwa na Maambukizi ya VVU sawa na asilimia 1.5

Sambamba na hilo, jumla ya Watoto 197 waliopima kipimo cha Kwanza cha VVU baada ya kuzaliwa ni Mtoto 1 pekee ndio alikutwa na Maambukizi ya VVU sawa na asilimia 0.5 Hii ina maana kwamba Mkakati wa kuzuia Virusi vya UKIMWI toka kwa Mama kwenda kwa Mtoto umeweza kuwakinga Watoto wasipatwe na Maambukizi ya VVU kwa asilimi 99.5

Akitoa taarifa ya matumizi ya dawa za ARV’s Mwasongwe amesema kuwa Jumala ya watu 291 kati ya 16,594 wanaotumia dawa za kufubaza makali ya Virusi vya UKIMWI wameripotiwa kutelekeza dawa jambo ambalo linasababisha kurudisha nyuma mapambano hayo sababu kuu zikitajwa kuwa ni imani za dini wanazoamishwa na Viongozi wa Dini kuwa wamepona.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudhibiti UKIMWI Filoteus Mligo amesema kuwa lengo la maadhimisho haya ni kutafakari na kuwakumbuka wenzetu waliopoteza maisha kutokana na ugonjwa huo na hivyo kuweza kutathmini na kuwa na mwelekeo na makusudi ya kutokomeza ugonjwa huo kwa kubaini changamoto na mafanikio na hivyo kuweka mikakati katika kupambana na kupunguza VVU na UKIMWI kwenye jamii zetu.

“Niwapongeze Halmashauri kwa kushirikiana na Wadau kwa kuhakikisha kuwa utekelezaji wa Malengo ya kupambana na UKIMWI ndani ya Halmashauri umefikia katika hatua nzuri. Katika Halmashauri yetu lipo jambo ambalo halifurahishi.Tumekuwa na tabia ya kufanya sherehe za kubwa wakati wa kujengea makaburi jambo hili limekuwa likifanyika kwa kutoa michango na sherehe kubwa lakini wakati tunauguza hatutoi michango kumsaidia mgonjwa mpaka anafariki.Tunafanya sherehe michango mikubwa tunaunda na Kamati na wakati anaumwa hatukumtilia maanani ila leo amefariki tunafanya sherehe ya kujenga makaburi.Utamaduni huu sio mzuri.Pia kunakuwa na miziki,ngoma watu wanacheza na kukesha mpaka asubuhi je hili haliwezi kuchangia UKIMWI?Tuache tabia na mila zisizo na maana katika jamii. Hili si jambo jema kwa jamii na hata mbele ya Mwenyezi Mungu”Alisema Mligo

Katika hatua nyingine Diwani wa Kata ya Ramadhan Nickson Nganyang’e amewataka Wazazi kuhakikisha kuwa Wanakuwa karibu na Watoto wao na kushirikiana katika malezi ya Watoto kwani kumekuwa na matukio makubwa ya Kikatili wanaofanyiwa Watoto ambao hupelekea watoto kuharibiwa Kisaikolojia na wakati mwingine kupata magonjwa ukiwemo UKIMWI.

Baadhi ya Wananchi walioshiriki katika Maadhimisho hayo akiwemo Joseph Fute na  Rosemary Athanaely wamesema kuwa ni wkati sasa jamii kuanchana na desturi ambazo hazina maadili katika jamii na pia wale wote waliopo katika matumizi ya dawa za kufubaza maambukizi kurudi na kuendlea na ufuasi wa dawa  ili kuendelea kuimarisha kinga zao.






Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe