• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

NJOMBE YAFANYA UZINDUZI WA KAMPENI YA CHANJO YA POLIO AWAMU YA TATU

Tarehe iliyowekwa: September 1st, 2022

Mkoa wa Njombe leo umefanya uzinduzi rasmi wa kampeni ya Chanjo ya Polio awamu ya tatu ambapo kupitia kampeni hiyo watoto 139,281 wenye umri chini ya miaka mitano wanataraji  kuchanjwa ili kujikinga na ugonjwa huo,uzinduzi uliofanyika katika kituo cha Afya Njombe Mjini na unatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku nne.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe amesema kuwa katika awamu zilizopita Mkoa wa Njombe uliweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa ambapo katika awamu ya kwanza Mkoa wa Njombe ulichanja kwa asilimia 116 na awamu ya pili asilimia 108.

Dkt. Grace Charles ni Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Kitengo cha  Chanjo ambapo amesema kuwa Njombe ni Miongoni mwa Mikoa ambayo imekua ikifanya vizuri na hii ni kutokana na ushirikiano ambao umekuwa ukiwepo na hivyo amewataka Wananchi kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo la chanjo.

Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Ayubu Mndeme akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Njombe kwenye Uzinduzi huo amesema kuwa chanjo hiyo ni muhimu kwani kwa Mtoto ambaye hajapatiwa chanjo ni hatari kwa maisha yake, wenzake, na jamii inayomzunguka  kwani anaweza kuambukiza au kuambukizwa ugonjwa kwa kutokuwa na kinga na hivyo kuwataka wahudumu wa afya kuhakikisha kuwa wanaimarisha usimamizi na utoaji huduma kwa kipindi chote.

"Nitoe rai kwa kwa Wananchi wote kuepuka upotoshaji kuhusiana na chanjo kwani chanjo hii ni ile ile ambayo hutolewa kwenye vituo vya huduma za afya katika ratiba ya kawaida ya chanjo.Ni salama na hutolewa bure hivyo kila mmoja wetu ahakikishe anakuwa mlinzi wa mwenzake."Alisema

Kwa upande wao baadhi ya wazazi ambao watoto wao walibahatika kupatiwa chanjo katika awamu zilizopita na leo hii wameshiriki kwenye uzinduzi huo wamesema kuwa chanjo hiyo ni muhumu kwani itawasaidia katika makuzi yao na hivyo kuwataka wazazi kupokea chanjo hiyo.Alisema Henela Busagala Mkazi wa Ramadhani 

Naye Agness Flowin Mkazi wa Njombe Mjini amwashauri wazazi na walezi kuachana na kauli potofu ambazo zinaweza kuhatarisha maisha na makuzi ya watoto wao kutokana na kukosa chanjo hiyo kwa kuwa na imani potofu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe