Kikao cha Kamati ya Ushauri na Maendeleo (RCC) Mkoani Njombe kilichoongozwa na Mkuu wa Mkao wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka Disemba 22,2023, kimeridhia kujengwa Tawi la chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) katika makao makuu ya Mkoa Mjini Njombe.
Akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe Profesa Lughano Kusiluka Makamu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) amesema katika utafiti wa maeneo ambayo yaliyoorodheshwa wamebaini kuwa maeneo ambayo yatafaa kwa ajili ya ujenzi wa chuo kikuu ni eneo la Shule ya Sekondari Njombe (NJOSS) na Ihalula yaliyopo Halmashauri ya Mji Njombe ,kutokana na maeneo hayo kukidhi vigezo kulingana miongozo ambayo inatakiwa kutumika.
Akiendelea kuzungumza Profesa Lughano amesema chuo kikuu cha Dodoma kitakachojengwa Njombe kitachukua kozi za ufugaji ,kilimo,Mawasiliano na teknolojia.
Anthony Mtaka Mkuu wa Mkoa wa Njombe amemshukuru Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha ambazo zita jenga chuo kikuu Mkoani Njombe huku akiwaomba wadau ambao wamehudhuria kikao hicho kutumai fursa mbalimbali za uchumi katika uwekezaji ambao utaleta ushindani wa uchumi.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Mhe.Deo Mwanyika na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhe Erasto Mpete kwa pamoja wamesema, wameridhiswa na maeneo ambayo yametengwa na kuchanguliwea kwa ajili ya ujenzi wa chuo kikuu jambo ambalo litaleta chachu ya maeneleo katika Mkoa wa Njombe.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe