Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Njombe Dkt. Jabil Juma amewaagiza wakuu wa vituo vya afya kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele kufuatilia utoaji wa huduma bora kwa wananchi ili kuweza kuleta tija.
Agizo hilo amelitoa Mei 29,2024 katika ukumbi wa Halmashauri ya mji kwenye kikao kazi cha kujadili taarifa za takwimu mbalimbali za huduma za afya kwa kipindi cha Januari mpaka Aprili mwaka huu.
Mganga Mkuu amesema wasimamizi wote wa vituo wanapaswa kutimiza wajibu wao wakusimamia hali ya utoaji wa huduma za afya sambamba na kuondoa malalamiko.
“Niwaombe viongozi wote wa vituo vya afya mmepewa mamlaka ya kusimamia wataalamu wa afya katika maeneo yenu nendeni mkatekeleze majukumu kama tulivowaamini,unakuwa kiongozi wa mahali tena wewe mwenyewe unakuwa huwajibiki haileti picha nzuri kwa halmashauri yetu” Alisema Mganga Mkuu Halmashauri ya Mji Njombe Dkt. Jabil Juma
Aidha amewasisitiza wakuu wa vituo vyote vya afya na zahanati kuhakikisha wanatenga bajeti ya mafuta kwa ajili ya gari la kubebea wagonjwa kwa mwaka fedha 2024/25.
“Sisi tunatoa huduma kwa wagonjwa, wakifika wamezidiwa na wanahitaji msaada wa rufaa ya kwenda hospitali kubwa mnakuwa hamna mafuta, niwaombe kila kituo mnatakiwa muwe na mafuta yenu na kusiwe na sababu ya kusema tumeshindwa kumsafirisha kwa sababu mafuta hayapo haitakubalika” amesema Dkt Juma.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe