• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

WAFANYABIASHARA TOENI RISITI.

Tarehe iliyowekwa: September 12th, 2023

Wafanyabiashara Mjini Njombe wametakiwa kutimiza wajibu wao wakutoa risiti baada huduma ili kuchangia mapato kwa maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa Septemba 11, 2023 na Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanyaiashara Taifa Ndugu Hamisi Livembe, kwenye mkutano na Jumuiya ya wafanyabiashara Mjini Njombe.

Livembe amesema Jumuiya imekuwa ikipokea kero kutoka kwa wafanyabiashara nakuziwasilisha kwa serikali lakini wafanyabiasha wamesahau wajibu wao wakutoa risiti halali jambo ambalo linapunguza mapato kwa serikali.

Amesisitiza kuwa ni vyema wafanyabiashara wakatambua kuwa haki huambatana na wajibu.

"Unapodai haki kumbuka kutimiza wajibu wako, wafanyabiashara mmejisahau baada ya kero zenu kusikilizwa na kufanyiwa kazi mmeacha kutoa risiti na hapa mnatuangusha maana inaonekana wazi mapato yameshuka na kwamba hampo tayari kutii sheria bila shuruti"

Ili kushughulikia changamoto hiyo amesema jumuiya imeandaa utaratibu wa kuwabaini wafanyabiashara ambao hawatoi risiti.

"Tumeandaa utaratibu na tutakuwa na kikosi maalamu ambacho kitapita nakukagagua machine kwa meizi  kadhaa na hapa tutawagundua tuu na tutahakikisha mnawajibika ili serikali isipoteze mapato."

Kwa upande wake meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania  (TRA) Mkoa wa Njombe Specioza Mickness Owure amewaonya wafanyabiasha wa mazao ya misitu mkoani Njombe  ambao wanatabia yakununua risiti feki.

Amesema tayari wamebaini njia zinazotumika na watachukuliwa hatua, ameeliza kuwa ni vyema wafanyabiashara wakafahamu  kuwa hakuna nchi inayoendeshwa bila mapato hivyo kutokulipa kodi ni kosa kisheria na nikukosa uzalendo na nchi haiwezi kuwa na maendeleo.

Aidha ametoa tahadhari kwa wananchi kutunza taarifa zao ikiwemo vitambulisho vyao vya taifa  (NIDA) ili visitumiwe vibaya kufanya udanganyifu kwenye masuala kodi.

"Wapo watu wamekuwa wanatumia namba za nida za watu, anakufata mtu anakuomba namba yako ya nida au kitambulisho unampatia kumbe anania ovu yakutengeneza namba ya mlipa kodi TIN kwa ajili yakutolea risiti feki jambo ambalo linaweza kukuingiza kwenye matatizo bila kufahamu,kuweni makini usitoe namba au kitambulisho chako bila kufahamu kinatumika kwa kazi gani."

Uongozi wa Jumuiya ya wafanyabiasha Tanzania unafanya ziara mikoa mbalimbali kwa lengo la kuangalia utulivu wa wafanyabiashara na kusikiliza kero mpya kutoka kwa wafanyabiashara ili ziweze kuwasilishwa  kwenye mamlaka husika nakupatiwa ufumbuzi , pia kutoa majibu ya baadhi ya kero ambazo ziliwalishwa kupitia kamati maalumu iliyoundwa na Mhe Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  ambazo tayari zimepatiwa majibu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ASILIMIA 100 WAFAULU KIDATO CHA SITA – MIUNDOMBINU WEZESHI NA MOTISHA YATAJWA KUWA CHACHU YA MAFANIKIO

    July 09, 2025
  • WATENDAJI WA VIJIJI NA MITAA WAPEWA MAFUNZO YA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI.

    July 05, 2025
  • RUZUKU YA CHANJO YA MIFUGO,KINGA KWA MAENDELEO YA MIFUGO

    July 05, 2025
  • Dkt. Mhede azindua zoezi la chanjo ya ruzuku kwa mifugo Halmashauri ya Mji Njombe, dozi 227,000 kutolewa kwa ng'ombe na kuku

    July 05, 2025
  • Angalia zote

Video

ZIFAHAMU FAIDA ZA HERENI YA KIELEKTRONIKI KWA NG'OMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe