• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

WANANCHI KATA YA UTALINGOLO WAFIKIWA NA ELIMU YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA.

Tarehe iliyowekwa: October 2nd, 2024

Wananchi wa kata ya Utalingolo Halmashauri ya mji wa Njombe wamepatiwa elimu ya uchaguzi waserikali za mitaa kutoka kwa maafisa uchaguzi wasiadizi wa kata na vijiji kwa kushirikiana na diwani wa kata hiyo Mhe.Erasto Mpete ambaye pia ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe .


Kata ya Utalingolo imekuwa kata ya kwanza kufikisha elimu hiyo mhimu kwa wananchi mabapo vijiji vyote vitatu vya kata hiyo vimefikiwa na wananchi kupata fursa ya kuuliza maswali katika mikutano iliyofanyika kwa siku mbili ambapo kijiji cha ihalula maafisa uchaguzi hao wametoa elimu katika kitongoji cha Nole.


Afisa msaidizi wa uchaguzi kata ya Utalingolo bwana Lenatus Mgani ambaye pia ni mtendaji wa kata  Hiyo amewataka wananchi kujitokeza kujiandikisha katika daftari maalumu amabapo uandikishaji utafanyika katika maeneo ya vitongoji wakiwa na vitambulisho vya aina mbalimbali ikiwemo vitambulisho vya nida

Ameanisha pia sifa za mpiga kura anayefika kujiandikisha katika fatari Maalumu la mpiga kura  kuwa ni pamoja na kua raia wa Tanzania,Awe mkazi wa kitongoji husika awe na akili timamu  mtu mwenye kipato awe na akili timamu na awe na umri wa kuanzia mika 18 na kuendelea

Katika hatua nyingine wananchi pia wamehamasishwa kujitokeza kugombea nafasi za uenyekiti wa kijiji ,uenyekiti wa kitongoji na ujumbe wa serikali ya halmashauri ya kijiji ambapo pia amebainisha sifa za anayetaka kuchaguliwa kua ni awe raia wa tanzania, awe na umri kuanzia miaka 21 na kuendelea, ajue kusoma na kuandika kiswahili au kingereza kwa ufasaha, awe na kipato halali cha kumuwezesha kuishi,aweni ni mkazi wa eneo husika, awe na akili timamu na awe mwanachama wa chama cha siasa,awe na akili timamu na awe amejiandikisha katika daftari maalumu la mpiga kura.  



Amesema kuwa uchaguzi serikali za mitaa utafanyika hapo tarehe 27 mwezi Novemba ambapo wagombea watafanya kampeni za kujinadi kwa wapiga kura  kwa muda wa siku sita Ambapo amewaomba wananchi kushiriki katika uchaguzi huo wa serikali za mita kwa amani na utulivu.


Diwani wa kata ya utalingolo ambaye pia ni mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Njombe Mhe.Erasto Mpete  akizungungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya kata ya utalingolo amewataka kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari maalumu la mpiga kura na Sanjari na   kuhakikisha wanawasikiliza na kuwaelewa wagombea na kisha kujitokeza kwa wingi kupiga kura hapo novemba 27 mwaka 2024 kwenye vituo vya kupigia kura ambavyo vitakuwa katika maeneo yao ya viongoji.


Amewataka wananchi kuwachagua viongozi wenye sifa njema wenye kujitolea katika shughuli mbalimbali za maendeleo na za kijamii ili waweze kuwaletea maendeleo katika nyanja mbalimbali.



Baadhi ya ananchi akiwemo vitalia mwajombe kutoka kijiji cha Ihalula na Grace Mpete kutoka kijiji cha  Utalingolo wameishukuru serikali hususani viongozi wa kata hiyo wakiongozwa na diwani wa kata hiyo Erasto Mpete ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa njombe kwa kuwahisha elimu hiyo ya uchaguzi.


‘’Sisi wananchi hii elimu ya uchaguzi tumeipokea vizuri na tunashukuru  Serikali kutufikia kwa upande wangu niko tayari kugombea na kuwapigia kura watakaogombea’’anabaisha Vitalia Mwajombe mkazi wa kijiji cha Ihalula. 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe