• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

WANANCHI MPOBOTA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

Tarehe iliyowekwa: October 11th, 2025

Wananchi wa Mtaa wa Mpobota, Kata ya Mjimwema,Halmashauri ya Mji Njombe wametakiwa kutumia haki yao ya kikatiba ifikapo Oktoba 29,2025 kwa kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi Mkuu wa kumchagua Rais,mbunge na diwani.


Akizungumza Oktoba 10,2025 na wananchi wa mtaa huo, Afisa Tarafa wa Njombe Mjini, Bi. Lilian Nyemele, aliwahimiza wananchi wote kujitokeza kupiga kura kwa amani na utulivu ili kuchagua viongozi wanaowataka ambao watawatumikia kwa uaminifu na uadilifu. Alisema kuwa kushiriki uchaguzi ni wajibu wa kila raia, kwa kuwa ni njia muhimu ya kuchangia maendeleo ya Taifa kupitia viongozi wanaochaguliwa kwa demokrasia.


Aliwakumbusha wananchi wote kuendelea kuhudhuria mikutano ya kampeni za wagombea wa nafasi mbalimbali, ili waweze kusikiliza sera, mipango na vipaumbele vyao kabla ya kufanya maamuzi wakati wa kupiga kura.


Alisisitiza umuhimu wa wananchi kutumia fursa hiyo kwa umakini na kutofanya maamuzi kwa misingi ya ushabiki au upendeleo, bali kwa kuzingatia uwezo na uwajibikaji wa mgombea.


Aidha, aliwakumbusha wananchi kuendelea kulinda amani na utulivu katika kipindi chote cha kampeni, siku ya kupiga kura na hata baada ya matokeo kutangazwa. Alisema kuwa tarafa ya Njombe Mjini imekuwa mfano wa amani kwa muda mrefu, hivyo hatarajii kusikia changamoto yoyote inayohusiana na uvunjifu wa amani au usalama.


“Ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa uchaguzi huu unafanyika kwa amani na utulivu. Tukiepuka maneno ya uchochezi na chuki, tutakuwa tumetoa mchango mkubwa katika kudumisha umoja na mshikamano katika jamii yetu,” alisema Nyemele.


Kwa upande wao, baadhi ya wananchi walieleza kuwa wako tayari kushiriki kikamilifu katika uchaguzi huo, huku wakiahidi kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha kuwa zoezi la uchaguzi linafanyika katika mazingira salama na tulivu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA YASISITIZWA KWA WAKULIMA WA MTAA WA MPOBOTA - MJIMWEMA .

    October 11, 2025
  • MWEKEZAJI MADEBE AKABIDHIWA HATI MILIKI 16

    October 11, 2025
  • WANANCHI MPOBOTA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 11, 2025
  • HERI YA SIKU YA MTOTO WA KIKE.

    October 11, 2025
  • Angalia zote

Video

IFAHAMU HUDUMA YA KIPEKEE INAYOPATIKANA NDANI YA SOKO KUU NJOMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe