Machi 3, 2025 ,Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya ya Njombe pamoja na menejimenti ya Halmashauri ya mji Njombe ,ilifanya ziara ya kukagua miradi itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru 2025.
Akizungumza katika ziara hiyo, mratibu wa Mwenge wa Uhuru wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Clemence Manga alieleza kuwa maandalizi yamefikia asilimia 85, hatua inayoashiria kuwa halmashauri iko tayari kwa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru.
Ziara hiyo ilianzia eneo la mapokezi lililopo kata ya Luponde, kijiji cha Madobole, ambako Mwenge wa Uhuru utapokelewa kutoka Wilaya ya Ludewa na baadaye kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya afya,elimu,viwanda na uwekezaji ,kilimo ,uhifadhi wa mazingira pamoja na kukagua vikundi vilivyonufaika na fursa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10 inayoyolewa na Halmashauri kwa vikundi vya wanawake vijana na watu wenye ulemavu
Halmashauri ya mji Njombe itapokea mwenge wa uhuru Tarehe 8 Mei ,2025.Kauli mbiu ya mbio za mwenge wa uhuru mwaka 2025 inasema ;"Jitokeze kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa amani na utulivu."
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe