Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe.Anthony Mtaka akizungumza kwenye Baraza maalumu la kujadili hoja za mdhibiti na mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) Juni 16,2025 pamoja na mambo mengine ametoa wito kwa Halmashauri ya mji Njombe kuchangamkia fursa za uwekezaji hata nje ya Halmashauri ili kuuendelea kuinua hadhi yake yakuwa makao makuu ya Mkoa wa Njombe.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe.Anthony Mtaka ametoa pongezi kwa waheshimiwa madiwani ambao wanamaliza kipindi chao cha uongozi baada ya miaka mitano akiwasisisitiza kutembea kifua mbele kwa kuwa kazi kubwa iliyofanywa na serikali kwenye maeneo yao imefanyika kipindi cha uongozi wao,hivyo wayaseme mafanikio hayo kwa wananchi.
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, Juni 12,2024 alifanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Mji Njombe na kueleza kuridhishwa na hatua zilizofikiwa kwenye miradi hiyo muhimu ya sekta ya elimu. Katika ziara hiyo, Mhe. Mtaka alitembelea ujenzi wa jengo la gorofa lenye vyumba 8 vya madarasa na ofisi 4 za walimu na matundu 4 ya vyoo katika Shule ya Sekondari Uwemba, mradi uliokadiriwa kugharimu zaidi ya shilingi milioni 600 hadi kukamilika.Pia alikagua ujenzi wa shule mpya ya Sekondari Wikichi unaotekelezwa kupitia programu ya SEQUIP kwa gharama ya shilingi milioni 583.
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe