• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

ACHENI KUFUATA USHAURI MTAANI - TUMIENI BIMA ZA AFYA VIZURI

Tarehe iliyowekwa: October 20th, 2023

Waalimu wa Shule za Sekondari Halmashauri ya Mji Njombe wameshauriwa kuepuka kupata ushauri wa kutumia dawa mtaani badala yake watumie bima ya afya kwenda kwenye vituo vya afya kuchunguzwa Afya zao ili kuepuka madhara yatokanayo na matumizi mabaya ya dawa bila kufuata ushauri wa wataalamu wa afya.

Rai hiyo imetolewa na mkaguzi wa dawa kutoka Mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA) kanda ya nyanda za juu kusini Bi Grace Kapande wakati akitoa elimu ya matumizi sahihi ya dawa na madhara yatokanayo na matumizi mabaya ya dawa kwa waalimu wa Shule za Sekondari Mabatini,Mbeyela ,Yakobi na Uwemba.

“Ninyi wote ni watumishi wa serikali na mna bima za afya niwaombe tumieni hizo bima kuchunguza afya zenu ,nenda hospitali usikubali ununue dawa bila kupima ugonjwa wakati bima ya afya unayo ,na uzuri sasa hivi kwenye hospitali zetu vipimo vingi vinafanyika tupime afya wapendwa”Alisema Bi Grace Mkaguzi wa Dawa kutoka TMDA.

Aidha Bi Grace amesema matumizi mabaya ya dawa ikiwemo kutokumaliza dozi na kutumia dawa bila kupima afya yamesababisha baadhi ya  dawa kuonekana hazifanyi kazi kwasababu tayari zimetengeneza usugu wa vimelea vya magonjwa na nyingine kuharibu kabisa viungo kwenye mwili wa binadamu.

“Unapopewa dozi ya dawa na mtaalamu hakikisha unamaliza ,kumekuwa na tabia mtu anapewa dawa akinywa dozi mbili anapata nafuu anaacha,hiyo ni mbaya ndiyo inasababisha vimelea vinakuwa sugu na ugonjwa kujirudiarudia,kama dozi ni kutwa mara 3 kwa siku tano hakikisha unatumia kila baada ya saa nane bila kupunguza wala kuongeza muda hayo ndiyo matumizi sahihi dawa”Alisisitiza  Bi Grace.

Kwa upande wake mwalimu wa Shule ya Sekondari Mbeyela Pulkeria Mlwale alitoa shukrani kwa TMDA kufanya mafunzo hayo nakutoa ombi kwa wafamasia wanatoa huduma kwenye vituo vya afya kuendelea kutoa elimu nakusisitiza wagonjwa kutumia dozi kwa usahihi ili kuepuka ugonjwa kujirudia na kuwa sugu.

“Elimu iliyotolewa imenigusa sana hasa kwenye muda sahihi wa kumaliza dozi ,niombe hawa wataalamu wa dawa wakati wakumpatia mgonjwa dawa watoe elimu na msisitizo ili tutumie dawa kwa usahihi kama mlivyoeleza madhara na makubwa”Alisema  Mwalimu Pulkeria

Katika hatua nyingine Bi Grace Kapande mkaguzi wa dawa kutoka TMDA ametoa rai kwa waalimu kwenye shule za sekondari zilizopo Halmashauri ya Mji Njombe kuendelea kutoa elimu waliyopatiwa kwa wanafunzi na jamii ili kuepuka madhara yatokanayo na matumizi mabaya dawa.

Elimu ya matumizi sahihi ya dawa imetolewa na TMDA  kwa waalimu na wanafunzi katika shule za sekondari Mpechi ,Mabatini,Mbeyela,Yakobi na Uwemba kuanzia Oktoba 18 ,2023 hadi Oktoba 20,2023.

Mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA) ni taasisi  ya serikali iliyopo chini ya wizara ya afya ,maendeleo ya jamii ,jinsia wazee na watoto yenye jukumu la kudhibiti ubora ,usalama,na ufanisi wa dawa ,vifaa tiba na vitendanishi ili kulinda afya ya jamii.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe