• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Halmashauri ya Mji Njombe
Halmashauri ya Mji Njombe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Halmashauri ya Mji Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

RC MTAKA AONGOZA MAOMBI YA AMANI KWA TAIFA.

Tarehe iliyowekwa: November 7th, 2025

Novemba 6, 2025,Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mheshimiwa Anthony Mtaka, ameongoza maombi maalum ya kuombea amani ya Taifa na Mkoa wa Njombe katika tukio lililofanyika eneo la stendi ya zamani katika Halmashauri ya Mji wa Makambako. 


Maombi hayo yalihudhuriwa na wananchi kutoka makundi mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara na wadau wa maendeleo. Tukio hilo lilitanguliwa na majadiliano yaliyoongozwa na Mhe. Mtaka kuhusu madhara yanayosababishwa na vurugu na vitendo vya uvunjifu wa amani.



Wananchi walipata nafasi ya kuelezea hisia zao kufuatia vurugu zilizojitokeza katika baadhi ya maeneo ya Tanzania Bara kipindi cha uchaguzi mkuu wa 2025 na baada yake, ambavyo vilisababisha uharibifu wa mali na athari kwa watu. 



Baadhi ya wafanyabiashara, akiwemo Bilnas Mtega, walizungumzia changamoto wanazokumbana nazo wakati shughuli za biashara zinasimama kutokana na vurugu, huku wakitoa pongezi kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Njombe kwa kuchukua hatua za mapema kukabiliana na viashiria vya uvunjifu wa amani. 



“Sisi machinga tunapambana kila siku ili familia ipate chakula, lakini unapokaa siku nne au tano bila kufanya kazi inaathiri sana maisha yetu,” alisema Mtega. 



Naye Jestina Singaile aliwataka wanawake kuendelea kuombea Taifa na viongozi, akisisitiza umuhimu wa kudumisha maombi na upendo ili kuzuia vurugu na chuki katika jamii. 



"Wanawake tuache kushabikia haya mambo ,hatuwezi sisi,tudumu katika maombi ,tukikaa magotini Mungu atatupa majibu sahihi ,tutafute amani na uzima ,tupendane tusinyoosheane  vidole,tudumu katika maombi nchi itakuwa salama"Alisema. 



Baada ya mjadala na maombi, Mhe. Mtaka aliwataka wananchi na wafanyabiashara wa Mkoa wa Njombe kuendelea kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa utulivu, akisisitiza kuwa matukio ya misukosuko yaliyotokea katika mikoa mingine yamepita na hayapaswi kuleta hofu. 



Alihitimisha kwa kutoa wito kwa wananchi wote kuendeleza mshikamano, upendo, na maombi kwa ajili ya kulijenga Taifa lenye amani na utulivu wa kudumu.


Matangazo

  • KUITWA KAZINI NA MAFUNZO TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI JIMBO LA NJOMBE MJINI. October 21, 2025
  • TANGAZO LA UCHAGUZI JIMBO LA NJOMBE MJINI. October 19, 2025
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTAKA AONGOZA MAOMBI YA AMANI KWA TAIFA.

    November 07, 2025
  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO NJOMBE MJINI AFUNGUA MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA .

    October 26, 2025
  • MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA 366 WAAPISHWA NA KUPATIWA MAFUNZO JIMBO LA NJOMBE MJINI.

    October 25, 2025
  • KUBWA KULIKO KUWAHI KUTOKEA NJOMBE MJINI

    October 20, 2025
  • Angalia zote

Video

TANGAZO LA UCHAGUZI JIMBO LA NJOMBE MJINI.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe