• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Halmashauri ya Mji Njombe
Halmashauri ya Mji Njombe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Halmashauri ya Mji Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

ASILIMIA 100 UANDIKISHAJI AWALI NA DARASA LA KWANZA

Tarehe iliyowekwa: January 17th, 2024


Shule ya msingi Nazareth iliyopo kata ya Mji Mwema Halmashauri ya Mji Njombe imefikia lengo la kuandikisha wanafunzi wa darasa la awali na darasa la kwanza kwa asilimia 100 mwaka 2024.


Akitoa taarifa ya shule hiyo Januari 17,2024 kwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe.Anthony Mtaka aliyefanya ziara shuleni hapo ,Mkuu wa shule ya Msingi Nazareth Mwalimu Onani Luponelo Myenda amesema malengo ya uandikishaji shuleni hapo yalikuwa ni kuandikisha  wanafunzi 84 wa darasa la awali na wanafunzi 109 wa darasa la kwanza na kwamba hadi sasa wamevuka lengo kwa kuandikisha na kupokea wanafunzi 86 wa darasa la awali na wanafunzi 128 wa darasa la kwanza.


Akizungumzia kuhusu taaluma shuleni hapo Mwalimu Myenda amesema, kiwango cha ufaulu kwa darasa la nne na darasa la saba kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2020 ni zaidi ya asilimia 90.


Aidha ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia shule hiyo fedha kiasi cha shilingi milioni 56 kwa kipidi cha mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na matundu matatu ya vyoo  kupitia mradi wa BOOST.


Akitoa takwimu za jumla za  uandikishaji wa darasa la awali na darasa la kwanza kwa halmashauri ya Mji Njombe Afisa Elimu Halmashauri ya Mji Njombe Bi.Shida Kiaramba amesema mpaka sasa darasa la awali wamepokelewa wanafunzi 3316 sawa na asilimia 71 yakundikisha wanafunzi  4639 na darasa la kwanza wamepokelewa wanafunzi 3924 sawa na asilimia 89 ya kuandikisha wanafunzi 4408. 



Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Bi Kuruthum Sadick amewahakikishia waalimu na wanafunzi wa  kuwa changamoto ya upungufu wa matundu ya vyoo shuleni hapo imefanyiwa kazi na mwaka wa fedha ujao 2024/2025 yataongezwa matundu 20 ili yatosheleze  kuhudumia wanafunzi wote shuleni hapo.


Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka,  amepongeza uongozi wa shule ya Msingi Nazareth na Halmashauri kwa namna ambavyo suala la  taalama linasimamiwa vizuri shuleni hapo.

Matangazo

  • KUITWA KAZINI NA MAFUNZO TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI JIMBO LA NJOMBE MJINI. October 21, 2025
  • TANGAZO LA UCHAGUZI JIMBO LA NJOMBE MJINI. October 19, 2025
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTAKA AONGOZA MAOMBI YA AMANI KWA TAIFA.

    November 07, 2025
  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO NJOMBE MJINI AFUNGUA MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA .

    October 26, 2025
  • MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA 366 WAAPISHWA NA KUPATIWA MAFUNZO JIMBO LA NJOMBE MJINI.

    October 25, 2025
  • KUBWA KULIKO KUWAHI KUTOKEA NJOMBE MJINI

    October 20, 2025
  • Angalia zote

Video

TANGAZO LA UCHAGUZI JIMBO LA NJOMBE MJINI.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe