• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

“BALOZI WA MTOTO” Programu inayolenga kumlinda mtoto Njombe

Tarehe iliyowekwa: January 16th, 2019

Akizungumza wakati wa mafunzo yaliyolenga kujenga uelewa wa pamoja kuhusu ulinzi na usalama wa mtoto katika Halmashauri ya Mji Njombe, Mkuu wa Wilaya ya Njombe Ruth Msafiri ameitaka jamii kutambua kuwa swala la ulinzi na usalama wa mtoto ni jukumu la jamii nzima  hivyo ni vyema  jamii kuzifahamu na kuzijua haki za mtoto na kuhakikisha kuwa inazilinda.

“Kumekuwa na matukio mengi ya ukatili kwa watoto kwa siku za karibuni yakiwemo ya kingono, kimwili, kutelekezwa, unyonyaji, usafirishaji haramu wa watoto, ukeketaji na ndoa za utotoni.  Matukio haya yanasikitisha sana, ni vyema tukaona namna ya kuanzisha balozi wa mtoto ambaye atakua rafiki wa watoto na ambaye atakuwa mwaminifu na mwadilifu, awe tayari kuonya na kukemea maovu yote yanayofanyika kwa watoto ambaye mtoto anapopatwa na tatizo aweze kumwelezea na afahamike katika jamii husika” Alisema Mkuu wa Wilaya.

Kwa mujibu wa sheria ya Mtoto namba 21 ya mwaka 2009 kifungu kidogo cha 5, inazipa mamlaka za serikali za mitaa mamlaka ya kulea, kulinda na kutunza watoto walioko katika Halmashauri zao. Hivyo ni wajibu wa madiwani wakiwa na mwenyeviti wao kama viongozi wa siasa kuhakikisha wanawalea watoto kutoka katika ngazi ya Kata hadi Halmashauri.

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Njombe George Emmanuel amesema kuwa ni vyema sheria inayolenga kutoa adhabu kwa serikali za mitaa kutotekeleza wajibu kulipa faini isiyozidi elfu hamsini, kifungo cha miezi mitatu au yote kwa pamoja kuangalia vyema na  kufanya mabadiliko ya sheria hii kulingana na Mazingira ya sasa kwani adhabu hii ni ndogo ukilinganisha na matatizo yanayoweza kujitokeza pale ambapo  Halmashauri inashindwa kutekeleza jukumu la kuwalinda watoto walioko kwenye Halmashauri zao.

Kikao hicho pia kimeazimia kuhakikisha kuwa Halmashauri inatenga fedha katika bajeti ijayo kuanzisha mchakato wa ujenzi wa kituo cha watoto kijulikanacho kama one stock Centre ambapo huduma za kisheria,kimalezi na huduma zote zinazomuhusu mtoto zitakuwa zinapatikana katika kituo hicho.

Hosea Yusto ni Afisa Ustawi Halmashauri ya Mji Njombe amesema kuwa kwa kipindi cha mwaka 2017/2018 kesi 54 za ukatili dhidi ya watoto zilifikishwa mahakamani  kwa upande wa Halmashauri ya Mji Njombe na Halmashauri imeanzisha mpango wa kutoa mafunzo kwa Wahe. Madiwani kuhusu kuzuia ukatili wa watoto lakini pia Halmashauri imepanga kuanzisha na kutoa mafunzo kwa timu za ulinzi wa mtoto na kuwapatia watoto mafunzo yatakayoweza kuwajengea uwezo wa kujilinda na kuwalinda wenzao.

Aidha, kupitia mafunzo hayo Halmashauri imelenga kuanzisha progamu ijulikanayo kama “Balozi wa Mtoto” itakayowezesha kupatikana kwa balozi kuanzia kila ngazi ikianzia familia mpaka kwenye Halmashauri ili kuweza kupata mabalozi watakaokuwa wasemaji wa watoto na kukemea ukatili dhidi ya watoto. Mafunzo hayo ya siku moja yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji njombe yaliwahusisha Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya, wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri pamoja na wadau mbalimbali.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe