Kwa mwaka wa fedha 2021/2022,Halmashauri ya Mji Njombe inakisia kukusanya Jumla ya Shilingi 37,844,106.191;Kati yake mapato ya ndani halisi ikiwa ni shilingi 4,763,050,980(Miradi ya Maendeleo Tsh 2,857,830,588, Mishahara 23,064,000 na Matumizi Mengineyo OC Shilingi 1,882,155,552;Ruzuku ya Mishahara (PE) Shilingi 22,533,546,000;Ruzuku ya Miradi ya Maendeleo Shilingi 7,020,665,211(Fedha za ndani Tsh 2,955,394,172 na Shilingi 4,065,270,039 ni fedha za nje wahisani;Ruzuku ya matumizi Mengineyo (OC) ni Shilingi 1,573,225,000 na Michango ya Wananchi ikiwa shilingi 1,953,620.000.
Wakichangia katika bajeti hiyo baadhi ya Waheshimiwa Madiwani Akiwemo Diwani wa Kata ya Makowo Honolatus Mgaya, Diwani wa Kata ya Matola Edwin Mwanzinga,Diwani wa Kata ya Luponde Ultrick Msemwa na Diwani wa Kata ya Mji Mwema Nestory Mahenge na Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika wameonesha kusikitishwa kwao na kutotumika ipasavyo kwa stendi ya mabasi Njombe na Soko Kuu Njombe licha ya Serikali kutumia fedha nyingi katika kufanikisha miradi hiyo jambo ambalo linaweza kuwa kikwazo kikubwa katika kufikia malengo ya makusanyo yaliyokadiriwa.
Mkutano huo umeridhia kwa pamoja kuhakikisha kuwa Wafanyabiashara wanaofanya Biashara zao katika maeneo yasiyo rasmi kuelekea katika maeneo ya masoko na kuwa na vituo vitatu vya kushusha na kupakia abiria ambavyo ni Nundu, Ramadhani na Kibena kama ilivyokuwa awali ili Halmashauri iweze kukusanya mapato na huduma ya stendi na soko ziweze kufanywa katika maeneo yaliyokusudiwa na Halmashauri na si kama hali ilivyo sasa ambapo maeneo ya barabarani yamegeuka kuwa masoko.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe