• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

BENKI KUU YA TANZANIA (BOT) YATOA MAFUNZO YA UWEKEZAJI KWENYE DHAMANA ZA SERIKALI KWA WATUMISHI MKOANI NJOMBE

Tarehe iliyowekwa: November 23rd, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Ndugu Judica Omari Novemba 23,2023 ,amefanya ufunguzi wa semina kwa watumishi wa umma Mkoani Njombe juu ya uwekezaji kwenye dhamana za serikali inayotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) tawi la Mbeya.

Bi Judica amesema mafunzo hayo yamekuja kwa wakati muafaka huku akiwataka washiriki kusikiliza kwa makini mafunzo hayo muhimu ambayo yatakuwa msaada kwa watumishi na serikali kwa kuwa uwekezaji kwenye dhamana za serikali ni salama na wenye faida kubwa kwa mwekezaji na kwa serikali kwa kuiwezesha kupata mapato.

Akizungumza wakati wa mafunzo Meneja fedha na Utawala kutoka BOT Tawi la Mbeya Bw. Agathon Kipandula, amesema semina hii ni mahususi kwa watumishi kuwahamasisha kuwekeza kwenye dhamana za Serikali. Aidha amesisitiza kuwa Uwekezaji huo ni salama na wenye faida kubwa hivyo watumishi watumie fursa hiyo kufanya Uwekezaji kidogo kidogo ili kuisaidia serikali kwenye mapato na kutekeleza majukumu kwa Maendeleo.

Benki kuu ya Tanzania kwa niaba ya serikali huuza dhamana za serikali ikiwa ni njia mojawapo ya kukopa fedha kutoka soko la ndani kwa makundi mawili ,dhamana za serikali za muda mfupi (Treasury bills) na dhamana za serikali za muda mrefu (Treasury bonds) ambazo huuzwa kwa njia yakufanya mnada kulingana na mpango wa ukopaji wa serikali kutoka masoko ya mahitaji ya ndani ya nchi, bila kuathiri mikopo kwa sekta binafsi.

Benki kuu ya Tanzania (BOT) ni benki ya Serikali yenye wajibu wakutunza fedha zote za serikali ,kukusanya mapato yote yatokanayo na dhamana za serikali na hati fungani pamoja na kulipa wadai na wawekezaji wote wa dhamana na hati fungani pia inazitumia dhamana za serikali na hati fungani kuleta uwiano kwenye ukwasi na ujazi wa fedha nchini Tanzania kama sehemu ya utekelezaji wa sera ya fedha.

Watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe na Halmashauri zote sita zinazounda mkoa wa Njombe wameshiriki semina hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe