• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

BILIONI 20.7 KUJENGA BARABARA ZA LAMI NJOMBE MJINI – MKANDARASI AKABIDHIWA SAITI KUANZA UJENZI

Tarehe iliyowekwa: July 24th, 2025

Serikali kupitia mradi wa TACTICS awamu ya pili inatarajia kutumia kiasi cha Shilingi Bilioni 20.7 kutekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami awamu ya kwanza katika Halmashauri ya Mji Njombe. Mkandarasi anayesimamia utekelezaji wa mradi huo China National Aero Technology International Engineering Corporation, amekabidhiwa rasmi maeneo ya ujenzi (saiti) Julai 23,2025 tayari kuanza kazi.

Mradi huo unahusisha ujenzi wa barabara zenye jumla ya urefu wa kilomita 8.4 zitakazojengwa kwa kiwango cha lami sambamba na uwekaji

wa miundombinu ya kisasa ikiwemo ujenzi wa ofisi ya mradi yenye gorofa moja,madaraja na taa za barabarani. Mkataba wa ujenzi una muda wa miezi 15, hivyo barabara zinatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba 2026.

Miongoni mwa barabara zitakazojengwa ni barabara ya NBC-Kibena km 2.84,Chaugingi - Nzengerendete - km 1.57,Nzengerendete-Masaki km 1.43

,Magereza-Matalawe km 1.12 na barabara ya Mpechi-Melinze KM 1.3

Baadhi ya wananchi waliokusanyika kushuhudia makabidhiano hayo katika maeneo mbalimbali ya mradi, wameishukuru Serikali kwa kuwaletea maendeleo na kuomba mkandarasi kuzingatia muda uliopangwa ili

kukamilisha mradi kwa wakati.

Kwa upande wake, Mhandisi Costastine Bengwe kutoka Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Njombe, ambaye ni msimamizi wa mradi huo, amesisitiza mkandarasi kuzingatia masharti ya mkataba na kufanya kazi kwa viwango vinavyostahili. Ameeleza kuwa TARURA iko tayari kutoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ubora na kwa wakati.

Mbali na maboresho ya miundombinu, mradi huo unatarajiwa kuleta fursa mbalimbali kwa wakazi wa Mji wa Njombe, ikiwemo ajira rasmi na zisizo rasmi kwa kipindi chote cha utekelezaji wa mradi.

“Tunategemea kuona si tu barabara bora, bali pia kuona wananchi wa hapa wakinufaika kiuchumi kupitia ajira zitakazopatikana,” amesema Mhandisi Costastine.

Mradi huu ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuimarisha miundombinu ya barabara, kuinua uchumi wa wananchi na kuboresha taswira ya miji kwa maendeleo endelevu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA YASISITIZWA KWA WAKULIMA WA MTAA WA MPOBOTA - MJIMWEMA .

    October 11, 2025
  • MWEKEZAJI MADEBE AKABIDHIWA HATI MILIKI 16

    October 11, 2025
  • WANANCHI MPOBOTA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 11, 2025
  • HERI YA SIKU YA MTOTO WA KIKE.

    October 11, 2025
  • Angalia zote

Video

IFAHAMU HUDUMA YA KIPEKEE INAYOPATIKANA NDANI YA SOKO KUU NJOMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe