Kata ya Mji Mwema Halmashauri ya Mji Njombe kwa kipindi cha Miaka 3 ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt .Samia Suluhu Hassan imetekeleza miradi ya maendeleo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 5.3.
Akiwasilisha taarifa Aprili 2 ,2024 taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo mtendaji wa kata ya Mji Mwema Theophil Mwinuka amesema kwa awamu ya Sita ya Uongozi wa awamu ya sita kata ya Mji Mwema imepata mafanikio makubwa kwenye sekta ya elimu ,afya ,maendeleo ya Jamii ,kilimo ,mifugo ,barabara ,umeme ,maji, na shughuli za utekelezaji wa afua za lishe, ambavyo vimefanya wananchi wa kata ya hiyo kufurahishwa na utendaji kazi wa Mhe Rais Samia Suluhu Hassan.
Akizungumza kwenye mkutano huo kwa niaba Mkuu wa wilaya ya Njombe Mhe Kissa Kasongwa, Afisa Tarafa ,Tarafa ya Njombe Mjini Lilian Nyemele ameompongeza Raisi wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania kwa kuleta fedha nyingi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo akiwataka wanachi kuendelea kuunga mkono jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali kuieletea nchi maendeleo.
Kwa Upande wake Diwani wa Kata ya Mji Mwema Mhe.Nestory Mahenge,ametumia fursa hiyo kuwaomba wazazi na walezi kuwapeleka watoto shule na kuona umuhimu wakuwapeleka bweni wanafunzi wa shule za sekondari ili waweze kufanya vizuri kwenye masomo yao.
Pamoja na kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika mkutano huo ilitolewa huduma ya kutoa vyeti vya kuzaliwa na vitambulisho vya taifa.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe