• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Bilioni 7.65 kuanza awamu ya pili ya ujenzi Hospitali ya Rufaa Njombe

Tarehe iliyowekwa: July 10th, 2019

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto amesema kuwa Serikali imetoa kiasi cha Shilingi Bilioni 7.65 kwa ajili ya kuanza rasmi hatua ya pili ya ujenzi wa majengo  kwa ajili ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

Hayo yamesemwa na Waziri Ummy wakati wa uzinduzi wa huduma katika Hospital mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe ambapo amezindua rasmi shughuli za utoaji huduma katika Hospitali hiyo. Uzinduzi huo uliambatana na kukabidhi iliyokuwa Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa Kibena kwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka ambaye naye aliikabidhi kwa uongozi wa Halmashauri ya Mji Njombe kwa ajili ya kuendelea na utaratibu wa kuiendesha Hospitali hiyo kama ilivyokuwa awali.

“Rais Magufuli ametupatia shilingi bilioni 7.65 kwa ajili ya hatua ya pili ya ujenzi wa hospitali hii mpya ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe hatua ambayo itahusisha ujenzi wa majengo mengine saba. Leo hapa ninamkabidhi eneo la ujenziwa majengo hayo Mkandarasi aanze kazi mara moja na ndani ya miezi 8 mpaka 10 awe amekamilisha ujenzi wa majengo hayo kwani fedha ipo ya kutosha. Serikali imepanga kuleta madaktari bingwa wa fani 13 pamoja na  vifaa vya kisasa kwa ajili ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.” Alisema Waziri Ummy.

Katika kuendelea kuboresha huduma za Afya Mkoani  Njombe Waziri Ummy ameuhakikishia uongozi wa Halmashauri ya Mji Njombe kuwa Hospitali ya Kibena itaendelea kutumia bajeti ya awali iliyokuwa inatumiwa ikiwa kama Hospitali Teule ya Rufaa ambayo ilikua ni  kiasi cha Shilingi milioni 280 na amesema kuwa hakuna kifaa tiba chochote kitakachoondolewa katika Hospitali ya Kibena kupelekwa katika Hospitali mpya ya rufaa.

“Napenda kuipongeza Halmashauri kwani hamkufanya makosa kukabidhi Hospitali ile ya Kibena itumike kama Hospitali ya Rufaa. Ninyi wenyewe ni mashahidi baada ya kuwa imeteuliwa kuwa Hospitali Teule ya Mkoa hali ya utoaji huduma ilibadilika kwa kiasi kikubwa. Ni matumaini yangu kuwa Halmashauri mtaendelea kuboresha utoaji huduma katika Hospitali ya Kibena ili ipatikane huduma bora zaidi na sisi tutaendelea kushirikiana na ninyi ili kuendelea kuihudumia” Waziri Ummy

Wakizungumza kwa wakati tofauti tofauti, baadhi ya Wananchi waliohudhuria katika uzinduzi wa huduma wameipongeza Wizara ya Afya na Serikali ya awamu ya tano kwa hatua wanazoendelea kuchukua za kuhakikisha kuwa huduma ya afya zinaboreka na kuimarika katika Mkoa wa Njombe kwani Mkoa wa Njombe, ni miongoni mwa Mikoa iliyokuwa inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa lakini sasa hali inaendelea kuboreka kila siku.

Ujenzi wa jengo la wagonjwa wa huduma za nje ambalo huduma katika jengo hilo imezinduliwa na Waziri Ummy imegharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 3.2 mpaka kukamilika kwake.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe