Jamii imehamasishwa kujitokeza kupata kinga tiba dhidi ya ugonjwa wa Usubi.
Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe kupitia Idara ya Afya na Ustawi wa jamii imeandaa zoezi la ugawaji wa kinga tiba dhidi ya ugonjwa wa usubi.
Wananchi wote kuaanzia watoto wenye umri wa miaka mitano(5) mnaombwa kujitokeza kupata kinga tiba hiyo.Zoezi hilo litafanywa na wagawa dawa ngazi ya jamii (CDD) nyumba kwa nyumba na kwenye vituo mbalimbali kuanzia Agosti 20,2023 hadi Agosti 27,2023.Vituo vitakavyotumika kutolea kinga tiba hizo ni pamoja na stendi kuu mpya ya mabasi ,stendi ya zamani,soko kuu,soko la wakulima na kwenye ofisi za halmashauri ya mji njombe zilizopo lunyanywi.
Akizungumza Agosti 11,2023 kwa niaba ya mganga mkuu wa Halmashauri ya Mji Njombe wakati akitoa elimu ya ugonjwa wa usubi kwa timu ya wataalamu wa Halmashauri ya Mji Njombe , Daktari Shella Myemba amesema takwimu za ugonjwa wa usubi mkoani njombe bado zipo juu na maeneo ya kata ya mji mwema , kijiji cha igola , kijiji cha itipula, mamongolo, kata ya kifanya ,madobole, kijiji cha mbega, kijiji cha idihani na St.Donbosco yanaongoza.
Ameeleza kuwa ugonjwa wa usubi ni ugonjwa wa kuambikiza unaosababishwa na nzi wadogowadogo waishio kandokando ya mito yenye maji masafi yanayotembea kwa kasi,nzi hao wanaweza kuruka kilomita 150 kwenda kueneza ugonjwa wakiwa na uwezo wakuachia minyoo midogomidogo elfu moja (1000) kwa siku ambayo inauwezo wa kuishi kwenye mwili wa binadamu kwa miaka kumi(10) hadi miaka kumi na tano (15).
Daktari Shella Myemba ameeleza athari za ugonjwa wa usubi kuwa ni pamoja na kuharibika vibaya kwa ngozi mithili ya ngozi ya kenge au mamba pamoja na kupata upofu wa kudumu
Kutokana na takwimu za sasa za ugonjwa wa usubi kuwa juu daktari Shella Myemba amesisitiza wale wote waliopatiwa dozi ya usubi mwezi machi 2023 , kurudia kupata dozi ya pili mara zoezi litakapoanza.
Njombe bila usubi inawezekana jitokeze kupata kinga tiba dhidi ya usubi.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe