Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mheshimiwa Kissa Gwakisa amewataka washiriki wa maonesho ya nane nane kutoka Wilaya ya Njombe kuendelea kutoa Elimu kwa jamii kuhusu shughuli wanazozifanya ili jamii kuendelea kunufaika na kujifunza.
Mheshimiwa Kissa ameyasema hayo wakati alipowatembelea Wakulima,wafugaji na wadau mbalimbali Wanaoshiriki katika maonesho hayo kutoka Halmashauri ya Mji Njombe na kuwapongeza kwa kazi ambazo zimewawezesha wao kushiriki katika maonesho hayo.
Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amewataka washiriki pia kujifunza kupitia kwa washiriki wengine ili kupata elimu,kubadilishana uzoefu na pia kwa yale ya kuvutia kuweza kuyatumia na kuyachukua kuboresha shughuli zao pindi warudipo Njombe.
Sambamba na hilo Kissa amewataka kuhakikisha wanatangaza fursa mbalimbali zinazopatikana katika Wilaya ya Njombe ili kuvutia makundi mbalimbali kuweza kutembelea katika Halmashauri hizo ikiwa ni Halmashauri ya Mji Njombe, Halmashauri ya Mji Makambako na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe