• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

DC Njombe aipongeza Njombe Mji kuwa vinara wa makusanyo na agenda ya Manispaa yapitishwa na Baraza la Madiwani

Tarehe iliyowekwa: July 30th, 2021

Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mheshimiwa Kissa Gwakisa ameipongeza Halmashauri ya Mji Njombe kwa kuwa kinara wa makusanyo kwenye Halmashauri za miji ambapo ameahidi kutoa ushirikiano na kuhakikisha Halmashauri Inaendelea kushikilia nafasi hiyo.

Akizungumza wakati wa kuwasilisha Salamu za Serikali katika Mkutano wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani kwa robo ya nne Kissa amesema kuwa Baraza la Madiwani,na Wataalamu wameomesha Ubunifu na Uzalendo wao katika kuhakikisha kuwa Halmashauri inafanya vizuri kwenye makusanyo.

"Ripoti ya Mheshimiwa Waziri kuhusu Makusanyo imedhihirisha wazi kuwa mnafanya Kazi. Napenda niwapongeze sana na niwaombe mkasimamie nafasi ambayo mmeipata. Zipo Halmashauri nyingine nazo zitakuja kwenye ushindani muhakikishe kuwa mnaishikilia nafasi hiyo.

Awali akitoa hotuba ya ufunguzi katika Baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri Erasto Mpete amesema kuwa Halmashauri imefanikiwa kuwa na zidio la makusanyo ya Shilingi Bilioni 1.5 na hii ikiwa ni kutokana na kuweza kuvuka Lengo la Makusanyo.

Katika hatua nyingine wakati wa kujadili taarifa za Kamati mbalimbali miongoni mwa hoja zilizojadiliwa kwa kina ni uanzishwaji wa Shule ya Msingi yenye mchepuo wa Kiingereza ambapo licha ya Kamati ya Uchumi Afya na Elimu kutoipa kipaumbele baadhi ya Madiwani wamesema hiyo ni kukatisha tamaa Wataalamu ambao wamekuwa wakihangaika kuandaa maandiko

“Wazo lilikuwa jema, Wataalamu wamekuwa wabunifu kuleta andiko hilo. Mimi ningeshauri kuwa wazo hilo kwa sasa lingesubiri kutokana na kwamba Halmashauri kwa sasa inamiradi mingi ya ujenzi na bado kuna Shule nyingi za Msingi zinahitaji kujengwa upya kutokana na miundombinu yake kuwa chakavu. Shule hii itahitaji Waalimu. tunachangamoto kubwa ya Waalimu. Hata Mimi katika Kata yangu hawajitoshelezi na tukianzisha Shule mpya itatubidi  Waalimu hao tulionao kuwagawa jambo ambapo tutakuwa tunawapa mzigo Waalimu. Mimi naona wazo ni jema ila lisubiri tukamilishe miradi hii mikubwa ambayo zaidi ya robo tatu ya michango yake ni nguvu ya Halmashauri.” Alisema Mwanzinga Diwani wa Kata ya Matola.

Katika Mkutano huo wa Baraza baadhi ya agenda mbalimbali ziliweza kujadiliwa ambapo Moja katika ya agenda iliyowasilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri Thadei Luoga ilikuwa ni ile ya Baraza la Madiwani kupitisha mchakato wa Halmashauri kuwa Manispaa.

Akiwasilisha agenda hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri alisema kuwa mara baada ya kupitia vigezo mbalimbali kubwa ikiwa ni ukusanyaji mapato imeona Halmashauri inafaa kupanda hadhi na kuwa Manispaa kwani inakidhi vigezo vilivyo vingi.

Wakichangia katika hoja hiyo baadhi ya Madiwani akiwemo Diwani wa Kata ya Matola Edwin Mwanzinga na Kata ya Ramadhani Nickson Nganyange wamesema kuwa licha ya kuwa wanaunga mkono hoja bado kuna ujenzi holela ndani ya Halmashauri,ujenzi wa mabanda ya Miti,uwepo wa makontena na ujenzi usiofuata mpango kabambe wa Halmashauri jambo linaloharibu taswira ya Mji.

"Tunaelekea kuwa Manispaa makontena yote yaliyopo mjini yanatakiwa yaondolewe. Kuna vibanda vya mbao kwa ajili ya biashara mbalimbali katika eneo la Mji hivyo vyote vinatakiwa viondoke ili Mji uwe na hadhi ya Manispaa. Hatuwezi kuwa Manispaa kila sehemu kuna vibanda Alisema Mwanzinga

Diwani wa Kata ya Mjimwema Nestory Mahenge amesema kuwa bado kuna maeneo ya mjini yana uwepo wa vichaka vinavyotumika kwa ajili ya uhalifu na matukio mbalimbali na hivyo ameomba wenye maeneo yao kuhakikisha yanasafishwa na kufanya ujenzi katika maeneo hayo kwani usafi wa Mji na mazingira yanayozunguka Mji Ni vigezo muhimu kwenye Manispaa.

Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika amesema kuwa kwa kipindi kirefu kumekuwa na mvutano wa kimaamuzi kati ta Wataalamu na Wanasiasa jambo lililopeleke kucheleweshwa kwa maendeleo katika Njombe.

“Hoja za Madiwani za Halmashauri kuwa Manispaa ni hoja za Msingi. Na kwenye Kampeni Wananchi waliomba Njombe kuwa Manispaa. Na tuliwaahidi kuhakikisha kulisimamia hilo na kuliwasilisha katika ngazi mbalimbali za maamuzi. Hoja yangu pia inajikita katika kuonesha mchango wa Njombe kwenye uchumi wa Taifa” Alisema Deo Mwanyika Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini

 Agenda ya Kuipandisha Halmashauri kuwa Manispaa iliungwa Mkono na Madiwani wote na sasa taratibu zinaendelea ili kuweza kufanikisha lengo Hilo




Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe