• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

ELIMU KUHUSU UMILIKI WA ARDHI YATOLEWA KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA MFEREKE

Tarehe iliyowekwa: June 12th, 2025

Juni 10, 2025 ,Wananchi wa kijiji cha Mfereke walipatiwa elimu ya umiliki wa ardhi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika ofisi za kijiji  kwa lengo la kupeana taarifa za maendeleo ya kijiji pamoja na kuwajengea wananchi uelewa kuhusu masuala ya ardhi kama njia mojawapo ya kuimarisha maendeleo ya kijiji.


Katika mkutano huo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ardhi na Mipango miji H/Mji Njombe, Emmanuel Luhamba alitoa elimu kuhusu masuala ya ardhi ikiwemo umuhimu wa kupanga, kupima na kumiliki ardhi kisheria pamoja na faida zake kiuchumi na kijamii. Elimu hiyo imelenga kuwajengea uelewa wakazi wa Mfereke kuhusu matumizi bora ya ardhi na nafasi ya ardhi katika kuinua kipato chao.


 "Kupanga na kupima ardhi ni hatua muhimu ya kuleta maendeleo ,inasaidia Umiliki halali wa ardhi na kumuwezesha mwananchi kupata mikopo, kuwekeza bila hofu, na kuhakikisha ardhi inatumika kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho," alisema Emmanuel Luhamba


Akizungumza katika mkutano huo, mmoja wa wananchi wa Mfereke anayeishi nje ya kijiji alitoa wito kwa wakazi wa Mfereke kuchangamkia fursa zilizopo katika maeneo yao.


“Changamkieni fursa za kiuchumi kwenye maeneo yenu. Ipeni elimu kipaumbele kwa sababu nchi yetu bado ni miongoni mwa nchi zinazotoa elimu kwa gharama nafuu. Wapelekeni watoto shule,” alisisitiza.

Aidha, aliwahimiza vijana kuchangamkia fursa katika sekta ya ardhi akieleza kuwa, “Kila muda unaopita haurudi utumieni kuzalisha mali.” Alisisitiza pia umuhimu wa mshikamano na ushirikiano kati ya wananchi na viongozi katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo.


Kwa upande wa usalama, alitoa rai kwa wananchi kudumisha ulinzi wa kijiji chao kwa kushirikiana kwa karibu. “Kijiji cha Mfereke kinajulikana kwa ulinzi, na hili ni muhimu ili mali zetu ziwe salama.”


Katika hatua ya kuunga mkono maendeleo ya kijiji,Herbeth nziku aliahidi kujitolea kugharamia kuweka mfumo wa umeme kwnye nyumba ya mwalimu akieleza kuwa umeme tayari umepita nyumbani kwake na yeye ni miongoni mwa wanufaika wa huduma hiyo.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kijiji Venance Ngole alitoa shukrani kwa wananchi wazawa wa Mfereke waliopo ndani na nje ya kijiji kwa kuendelea kuonyesha moyo wa uzalendo na kukumbuka walikotoka. Alisisitiza kuwa mshikamano wa jamii hiyo utaendelea kuwa nguzo muhimu ya mafanikio yao ya kijamii na kiuchumi.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • ASILIMIA 100 WAFAULU KIDATO CHA SITA – MIUNDOMBINU WEZESHI NA MOTISHA YATAJWA KUWA CHACHU YA MAFANIKIO

    July 09, 2025
  • WATENDAJI WA VIJIJI NA MITAA WAPEWA MAFUNZO YA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI.

    July 05, 2025
  • RUZUKU YA CHANJO YA MIFUGO,KINGA KWA MAENDELEO YA MIFUGO

    July 05, 2025
  • Dkt. Mhede azindua zoezi la chanjo ya ruzuku kwa mifugo Halmashauri ya Mji Njombe, dozi 227,000 kutolewa kwa ng'ombe na kuku

    July 05, 2025
  • Angalia zote

Video

ZIFAHAMU FAIDA ZA HERENI YA KIELEKTRONIKI KWA NG'OMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe