• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

ELIMU YA MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA NA MBEGU YAWAFIKIA WANANCHI WA NGALANGA NA ULIWA

Tarehe iliyowekwa: October 9th, 2025

Kuelekea msimu wa kilimo wa mwaka 2025/2026, Idara ya Kilimo Halmashauri ya Mji wa Njombe Oktoba 08,2025 imetoa elimu ya matumizi sahihi ya mbolea na mbegu bora kwa wakulima katika vijiji vya Ngalanga na Uliwa, vilivyopo katika Kata ya Iwungilo.Pamoja na elimu hiyo wakulima hao walifundishwa mbinu bora za utunzaji wa ardhi kwa ajili ya kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao.


Afisa Kilimo, Ndg.Baraka Mlawa, alieleza kuwa lengo la elimu hiyo ni kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji kwa kutumia njia bora na sahihi za kilimo akitoa wito kwa wakulima wa zao la parachichi kuwa wavumilivu wakati wa kuuza mazao yao, kwani wengi huuza kwa bei ya chini sana inayowasabahishia hasara.


Wakulima hao walikumbushwa kununua mbolea kutoka kwa mawakala waliothibitishwa vijijini kwa bei elekezi, na kuwasilisha taarifa kwa viongozi wa kijiji, kata au wataalamu wa kilimo endapo watakutana na changamoto yoyote kuhusu upatikanaji au bei ya pembejeo hizo.


Wananchi walionufaika na elimu hiyo walitoa shukrani zao kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa kuhakikisha wataalamu wa kilimo wanawafikia wakulima moja kwa moja vijijini na kuwapatia elimu muhimu kuhusu kilimo bora, bei sahihi ya mbolea na mazao kama parachichi, jambo ambalo litasaidia kupata tija kwenye kilimo wanachofanya.

Walieleza kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakitumia mbolea bila uelewa sahihi wa matumizi yake, hali iliyochangia uzalishaji usioridhisha. Aidha walitoa ombi kwa Serikali na wataalamu wa kilimo kuwasaidia kupima udongo ili waweze kulima kwa kuzingatia aina ya udongo na mbegu zinazofaa.


“Tunashukuru sana kwa elimu hii. Huku vijijini tumekuwa tukilima kwa mazoea bila kufuata taratibu za kilimo bora. Tunaomba Serikali itupe msaada wa kupima udongo ili tujue ni mbegu gani zinafaa, maana wakati mwingine tunapanda mazao hayazai kama tunavyotarajia, hatujui kama shida ni mbegu au mbolea,”. Alisema mmoja wa wakulima wa Kijiji cha Ngalanga.


Elimu hiyo inaendelea kutolewa katika maeneo mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Mji Njombe.


#maendeleokwawote 


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

    October 15, 2025
  • MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA YASISITIZWA KWA WAKULIMA WA MTAA WA MPOBOTA - MJIMWEMA .

    October 11, 2025
  • MWEKEZAJI MADEBE AKABIDHIWA HATI MILIKI 16

    October 11, 2025
  • WANANCHI MPOBOTA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 11, 2025
  • Angalia zote

Video

IFAHAMU HUDUMA YA KIPEKEE INAYOPATIKANA NDANI YA SOKO KUU NJOMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe