• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Halmashauri ya Mji Njombe
Halmashauri ya Mji Njombe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Halmashauri ya Mji Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

ELIMU YA WATU WAZIMA IJIELEKEZE KWENYE MITAALA MIPYA.

Tarehe iliyowekwa: September 9th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, amewataka Maafisa Elimu ya Watu wazima mkoa wa Njombe kujielekeza katika mitaala mipya ya elimu ili kuendana na mabadiliko ya kidijitali na mahitaji ya  sasa kwenye jamii. 


Akizungumza Septemba 8, 2025, katika maadhimisho ya wiki ya Elimu ya watu wazima mkoa wa Njombe, Mhe. Mtaka amewataka maafisa elimu kuhakikisha wanaandaa mafunzo yanayoendana na mitaala ya sasa, kwa kuzingatia kasi ya kidijitali. Amesema elimu hiyo inapaswa kuwajengea wanafunzi ujuzi wa ujasiriamali, matumizi ya TEHAMA na mbinu za kujiongezea kipato ili kupunguza umasikini na kukuza maendeleo ya jamii. 


Aidha, amewataka wazazi na walezi kuhakikisha watoto wote waliokosa fursa ya kusoma kwa changamoto mbalimbali, ikiwemo wale waliopata ujauzito wakiwa shule, wanarejea shule. 


“Hatuwezi kumzuia mtoto kwenda shule katika dunia ya sasa ya kidijitali. Vilevile, hatuwezi kuendelea na mitaala ya watu wazima inayopitwa na wakati. Tunapaswa kuhakikisha elimu ya watu wazima inajikita kwenye stadi zitakazosaidia wananchi kuishi na kufanya kazi katika karne hii ya teknolojia,” alisema Mhe. Mtaka. 


Kwa upande wake, Afisa Elimu ya watu wazima Mkoa wa Njombe, Fadhili Msilu, amesema mkoa wa Njombe unaendelea na utoaji wa Elimu ya Msingi kwa waliokosa (MEMKWA) ambapo kwa sasa kuna wanafunzi 201 wanaopatiwa masomo hayo. Aidha, kwa wale wenye mahitaji maalumu katika shule za msingi na sekondari, idadi imefikia wanafunzi 7,513. 


Ameongeza kuwa kwa sasa elimu ya watu wazima hutolewa kwa njia ya kidijitali tofauti na zamani ambapo mtu mzima alilazimika kufika shuleni au kutumia barua kwa njia ya posta. Mfumo huu mpya umeongeza fursa kwa watu walioko kazini au vijijini mbali na shule kuendelea kusoma bila kuathiri shughuli zao za kila siku. 


Maadhimisho ya Elimu ya watu wazima kwa mwaka 2025 yamebeba kauli mbiu isemayo: “Kukuza Kisomo Katika Zama za Kidijitali.”


#maendeleokwawote

Matangazo

  • KUITWA KAZINI NA MAFUNZO TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI JIMBO LA NJOMBE MJINI. October 21, 2025
  • TANGAZO LA UCHAGUZI JIMBO LA NJOMBE MJINI. October 19, 2025
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTAKA AONGOZA MAOMBI YA AMANI KWA TAIFA.

    November 07, 2025
  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO NJOMBE MJINI AFUNGUA MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA .

    October 26, 2025
  • MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA 366 WAAPISHWA NA KUPATIWA MAFUNZO JIMBO LA NJOMBE MJINI.

    October 25, 2025
  • KUBWA KULIKO KUWAHI KUTOKEA NJOMBE MJINI

    October 20, 2025
  • Angalia zote

Video

TANGAZO LA UCHAGUZI JIMBO LA NJOMBE MJINI.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe