Watendaji wa kata za Halmashauri ya Mji Njombe wametakiwa kuendelea kuhamzsisha na kutoa elimu ya lishe bora kwa wananchi ili kufanikisha kampeni yakupunguza udumavu mkoani Njombe.
Akizungumza Fabruari 28,2024 katika kikao cha utekelezaji wa viashiria vya mkataba wa lishe kwa kipindi cha robo ya pili Katibu Tawala Walaya Njombe Ndugu Agatha Mhaiki ametoa msisitizo kwa watendaji wote wa kata kwenda kuhamasisha viongiozi wote wa vijiji na mitaa kutoa elimu ya lishe ,kwa kuanda mikutano mbalimbali ya elimu kuhusu lishe ,elimu ya vitendo juu ya kuanda mlo kamili kwa watoto pamoja na umuhimu wa kuzingatia lishe yenye mchanganyiko wa makundi yote ya vyakula.
Kwa upande wake afisa lishe wa Halmashauri ya mji Njombe Fransisca Mosha amesema kutokana na juhudi ambazo wamekuwa wakizifanya za kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya lishe wameweza kuwa fikia Wazazi wa watoto wenye umri wa miezi 0 hadi 23 waliopata unasihi wa ulishaji wa watoto wachanga na wadogo kutoka kwa watoa huduma za afya ngazi ya vituo ,kuwapa watoto miezi 6 hadi 59 matone ya vitamini A wakati wa kampeni mbalimbali pamoja na watoto wenye umri chini ya miaka mitano waliogundulika kuwa na utapiamlo mkali kuanzishiwa dawa.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe