Wataalamu wa vituo vya afya ,zahanati na Hospitali Halmashauri ya mji Njombe wakumbushwa kutekeleza majukumu yao kwa wakati na uadilifu ili kuendana na kasi ya Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ambayo anaifanya ya kwenye sekta ya afya.
Akizungumza katika kikao cha Kujadili taarifa mbalimbali za huduma ya afya Oktoba 26 ,2023 kwa mwezi Septemba zinazotolewa katika maeneo Yao, Mganga mkuu halmashauri ya mji Njombe Dkt.Jabil Juma amewaomba Wataalamu hao wa afya halmashauri ya mji Njombe kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii na kufuata miongozo ya utendaji kazi.
Akiendelea kuzungumza katika kikao kazi hicho Dkt Juma amewataka wataalamu hao wa afya kwenda kuzifanyia kazi changamoto za utoaji huduma ambazo zimejitokeza kwa baadhi ya vituo vya afya na zahanati.
“Lengo la kukutana hapa kuangalia wapi Pana changamoto na nini kifanyike ili tuweze kuyafikia malengo yetu katika utoaji wa huduma kwa wanachi sasa tukitoka hapa kila moja wetu akafanye kazi kwa bidi ili tuweze kuzimaliza changamoto ambazo tunazo” Dkt.Jabil Juma.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe