• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

GARI JIPYA LA WAGONJWA LAKABIDHIWA KITUO CHA AFYA IHALULA

Tarehe iliyowekwa: January 8th, 2025

Tarehe 07 Januari 2025,Kituo cha Afya Ihalula kilichopo Kata ya Utalingolo Halmashauri ya Mji wa Njombe, kimepokea gari jipya la kubebea wagonjwa  (Ambulance).

Gari hilo limekabidhiwa rasmi na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini, Deo Mwanyika ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuboresha huduma za afya na kuwahudumia wananchi kwa haraka zaidi wakati inapotokea dharura.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mheshimiwa Mwanyika amesema kuwa gari hilo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi alizozitoa kwa wananchi wa kata ya Utalingolo.


"Tangu ziara yangu ya kwanza nilipofika hapa moja ya changamoto mlizoniambia nakuniomba haswa akina mama ni gari la wagonjwa wa dharura, nilitoa ahadi na diwani wenu amekuwa akinikumbusha mara kwa mara na leo ninafurahi kuwa ahadi imetimia," amesema Mhe.Mwanyika.


Kuhusu matumizi na utunzaji wa gari hilo Mheshimiwa Mbunge amesisitiza gari hilo ni kutumika kwenye kazi iliyokusudiwa.

"Gharama ya gari hili ni shilingi Milioni 250, gari hili ni gari kwa ajili ya shughuli maalumu kama tulivyoelezwa siyo la kutembelea au kuzururia siyo kwa ajili ya kufanya kazi tofauti na mahitaji yake. Hili gari ni la kwenu kwa maana ya kwamba wote tunajukumu la kulitunza," amesisitiza Mhe. Mwanyika.


Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Mhe. Erasto Mpete amewashukuru viongozi wa Serikali hususani Mhe.Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika kwa kusikiliza kilio cha wakazi wa Kata ya Utalingolo na kuwezesha upatikanaji wa gari hilo na amesisitiza gari hilo kutunzwa ili liweze kudumu na kuwahudumia wananchi kwa muda mrefu.


"Vizazi vyetu na vinavyofuata wanatakiwa wanufaike na hili gari kwa hiyo tuombe ushirikiano baina ya wataalamu na wananchi na mganga mfawidhi wa kituo tunaomba hili gari litunzwe," amesisitiza Mhe. Mpete.


Kwa upande wao wananchi wa Kijiji cha Ihalula walitoa shukrani zao dhati kwa Serikali na Mbunge wao kwa kutambua hitaji lao la muda mrefu na kulitekeleza.


Hafla ya kukabidhi gari hilo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali, wakiwemo waheshimiwa madiwani kutoka kata nyingine za Halmashauri ya Mji Njombe.


Gari hilo la wagonjwa litatoa huduma katika kata ya Utalingolo na kata nyingine za jirani kulingana na uhitaji wa eneo husika.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe