• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

HABARI NJEMA KUHUSU LISHE YAWAFIKIA WANANCHI WA ULIWA ,MASHINE YA KUONGEZA VIRUTUBISHO KUFUNGWA KIJIJINI HAPO

Tarehe iliyowekwa: October 10th, 2025

Wananchi wa Kijiji cha Uliwa, Kata ya Iwungilo, Halmashauri ya Mji wa Njombe, Oktoba 08,2025 wamepokea habari njema kufuatia mpango wa kufungwa kwa mashine ya kuongeza virutubishi kwenye unga, iliyotolewa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na mdau wa maendeleo, kampuni ya Sanku.


Mashine hiyo ni miongoni mwa tatu zilizotolewa kwa ajili ya kuchanganya virutubishi muhimu kama madini ya chuma na zinki kwenye unga wa mahindi, na itafungwa katika Kijiji cha Uliwa ili kuwahudumia wananchi kwa lengo la kupambana na utapiamlo na udumavu katika jamii.


Pamoja na taarifa ya uwekaji uwekaji wa mashine hiyo, wananchi pia wamepatiwa elimu ya lishe bora inayolenga kuboresha afya kupitia ulaji wa chakula chenye virutubishi vya kutosha na kuzingatia makundi yote ya vyakula.


Elimu hiyo imetolewa na Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Ndg.Michael Sway, katika mkutano uliofanyika kijijini hapo, ambapo alieleza kuwa mashine hizo zitafungwa katika vijiji vya Uliwa, Utalingolo pamoja na Mtaa wa Ramadhani.


“Kupitia mashine hizi, wananchi watanufaika na unga wenye mchanganyiko wa virutubishi muhimu, hasa madini ya chuma na zinki. Virutubishi hivi husaidia kuongeza nguvu mwilini, kusaidia ukuaji wa mifupa, kulinda afya ya mama mjamzito, na hata kuzuia mimba kuharibika,” alisema.


Aidha, aliwasisitiza wakina mama wajawazito na wale wenye watoto wachanga kuwa miongoni mwa walengwa wakuu wa huduma hiyo, kwa kuwa wao wako katika makundi yanayohitaji virutubishi kwa kiwango kikubwa zaidi kwa ajili ya afya ya mama na mtoto.


Matumizi ya vyakula vilivyoboreshwa kwa virutubishi ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa kupambana na tatizo la lishe duni na udumavu, hasa katika maeneo ya vijijini ambako upatikanaji wa chakula mchanganyiko unaweza kuwa changamoto kubwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

    October 15, 2025
  • MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA YASISITIZWA KWA WAKULIMA WA MTAA WA MPOBOTA - MJIMWEMA .

    October 11, 2025
  • MWEKEZAJI MADEBE AKABIDHIWA HATI MILIKI 16

    October 11, 2025
  • WANANCHI MPOBOTA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 11, 2025
  • Angalia zote

Video

IFAHAMU HUDUMA YA KIPEKEE INAYOPATIKANA NDANI YA SOKO KUU NJOMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe