• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Hali ya maambukizi ya VVU Njombe bado kizungumkuti,Wazazi wahimizwa kutoa taarifa kwa waalimu juu ya afya za watoto wao

Tarehe iliyowekwa: August 30th, 2018

Hayo yamesemwa na waalimu wa shule mbalimbali katika Halmashauri ya Mji Njombe, wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya wanafunzi wanaoishi na VVU yalioendesha na shirika la watu wanaoishi na VVU Njombe wakishirikiana na Mratibu wa Ukimwi Halmashauri ya Mji Njombe.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti waalimu hao wamesema kuwa wazazi wengi wamekuwa hawatoi taarifa juu ya afya za watoto wao jambo ambalo limekuwa likiwafanya waalimu kutojua afya za watoto pindi wawapo shuleni.

“Wanafunzi wanaoishi na VVU wanakumbwa na changamoto nyingi ikiwemo unyanyapaa. Kutokana na kuwa waalimu hususani waalimu wa malezi  wanakuwa hawana taarifa sahihi za mwanafunzi. Unaweza ukawa umemwadhibu mtoto kwa kutofika shuleni kumbe alienda kuchukua dawa, lakini huna taarifa mzazi hajakushirikisha chochote na hufahamu lolote. Wakati mwingine tunapokuwa tunataarifa inasaidia hata kuona ni kwa namna gani unamsaidia mwanafunzi husika.”Alisema Herry ambaye ni Mratibu Elimu Kata ya Mjimwema.

Herr aliongezea kuwa kujua afya ya mwanafunzi kunamsaidia mwalimu katika kupanga ratiba ya majaribio na mitihani mbalimbali bila kuingiliana na ratiba za wanafunzi wanaochukua dawa lakini pia kumpatia ruhusa mwanafunzi pindi anapotaka kwenda kuchukua dawa. Aidha taarifa hizo za afya zinawawezesha waalimu kutoa ushauri wa kiafya kwa wanafunzi kwa kuzingatia lishe bora.

Kwa wakati huo huo, Mratibu huyo wa Elimu amewataka waalimu kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa weledi na kuacha kujihusisha kimapenzi na wanafunzi kwani jambo hilo ndio limeibua hofu miongoni mwa wazazi kwa kukosa uaminifu na waalimu kutokana na kuwepo na kesi nyingi zinazowahusisha waalimu kuwa na mahusiano ya kimapenzi wa wanafunzi wao na kuwataka waalimu kuwa mstari wa mbele kuwasaidia wanafunzi kimalezi.

Mwalimu Steven Mwakila ambaye ni mwalimu wa malezi Mpechi Sekondari amewaomba viongozi wa dini kuhubiri maswala ya UKIMWI kwenye nyumba za ibada kwani janga hili sasa limeenda mbali zaidi katika Mkoa wa Njombe na sasa wanafunzi wengi wamekuwa wakijiingiza kwenye vitendo vya ngono jambo ambalo linachangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa maambukizi ya VVU.

Miongoni mwa mambo yaliyoibuliwa ni ugumu wa maisha katika ngazi za familia  sambamba na wazazi wengi kujihusisha zaidi na shughuli za kimaendeleo na kusahau elimu ya malezi kwa watoto jambo ambalo linapelekea watoto wengi kujiongoza wenyewe kimalezi. Wazazi wamehimizwa kutoa taarifa juu ya afya za watoto wao kwa waalimu badala ya kufanya siri kwani kunadidimiza maendeleo ya mtoto shuleni lakini pia wazazi kuwa karibu na watoto wao kwa kufuatilia maendeleo yao shuleni lakini pia nidhamu za watoto pindi wawapo shuleni badala ya watoto kujiongoza wenyewe na kufanya maamuzi ya maisha yao wenyewe jambo ambalo linawaingiza wengi katika makundi yasiyofaa na kupelekea mmomonyoko wa maadili.

Takwimu zinaonyesha kuwa kwa upande wa Halmashauri ya Mji Njombe, Wanafunzi 229 katika shule za msingi wanaishi na VVU na wanafunzi 62 ikiwa ni katika shule za Sekondari.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe