• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAENDELEA KUPIGA HATUA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE .

Tarehe iliyowekwa: July 29th, 2025

Halmashauri ya Mji Njombe imeendelea kung’ara katika utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2024/2025, kwa kufanikisha utoaji wa huduma muhimu za lishe kwa makundi mbalimbali ya wananchi.


Afisa Lishe wa Halmashauri Bw. Michael Swai amesema mafanikio makubwa yamepatikana katika viashiria vyote muhimu vya mkataba wa lishe katika kipindi cha robo ya nne 2024/2025.


Bw. Swai ameeleza kuwa utoaji wa elimu na unasihi wa ulishaji wa watoto wachanga na wadogo wenye umri wa miezi 0 hadi 23 ulifanyika kwa mafanikio makubwa, ambapo lengo lilikuwa kuwafikia akina mama 2,484 lakini waliopatiwa elimu hiyo walifikia 3,716, sawa na asilimia 100 ya lengo lililowekwa.


Aidha, huduma ya unasihi katika vituo vya kutolea huduma za afya iliwafikia watu 20,700 ambao ndio walengwa waliopangwa, huku huduma ya utoaji wa vidonge vya kuongeza damu kwa wanawake wajawazito waliokuwa wakihudhuria kliniki nazo zikitolewa kikamilifu kwa wanawake 8,241 sawa na asilimia 100 ya waliotarajiwa.



Katika kuhakikisha watoto wanapata kinga dhidi ya upungufu wa vitamini A, watoto 22,028 wenye umri wa miezi 6 hadi 59 walipatiwa matone ya vitamini A, zaidi ya lengo la awali la watoto 21,110, sawa na asilimia 100 ya utekelezaji.


Kwa upande wa matibabu ya utapiamlo mkali, watoto 5 chini ya miaka 5 walipokelewa katika kipindi hicho, ambapo watoto 4 walipona na mmoja alifariki dunia.



Katika jitihada za kuhamasisha jamii kuhusu lishe bora, Bw. Swai amesema kuwa vijiji na mitaa yote katika Halmashauri hiyo vilifanya maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji, huku ikiripotiwa ongezeko la ushiriki wa wanaume katika shughuli hizo jambo ambalo awali lilikuwa changamoto kubwa katika kampeni za lishe.


Halmashauri ya Mji Njombe bado inaendelea na juhudi za makusudi kukabiliana na changamoto za udumavu, uzito pungufu na uzito uliozidi kwa watoto chini ya miaka mitano. Takwimu zinaonesha kuwa hadi kufikia robo ya nne ya mwaka 2024/2025, kiwango cha udumavu kimefikia 42.4%, uzito pungufu 9.4%, na uzito uliozidi 9.0%.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI NJOMBE TC AAGANA NA TIMU ITAKAYOCHEZA SHIMISEMITA.

    August 12, 2025
  • LISHE NA AKIBA YA MAZAO YAHIMIZWA NANENANE.

    August 08, 2025
  • KHERI YA SIKUKUU YA WAKULIMA 88 2025.

    August 08, 2025
  • ELIMU YA UNYONYESHAJI YATOLEWA KWA WAKAZI WA LWANGU

    August 05, 2025
  • Angalia zote

Video

ZIFAHAMU FAIDA ZA HERENI YA KIELEKTRONIKI KWA NG'OMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe