Halmashauri ya Mji Njombe imepongezwa kwa kuwa na usimamizi bora wa rasilimali fedha ulioiwezesha kupata hati safi kutoka kwa mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2021/2022.
Pongezi hizo zimetolewa Juni 19,2023 na Katibu Tawala Mkoa wa Njombe Judica Omari kwenye mkutano maalumu wa baraza la waheshimiwa madiwani lililokaa kupitia na kujadili hoja za mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2021/2022.
Ameeleza kuwa ukusanyaji na usimamizi mzuri wa mapato kwa Halmashauri ya Mji Njombe ambao mpaka umefikia asilimia 96% umeuwezesha mkoa kwa kiasi kukubwa kufikia lengo na kwamba hana wasiwasi hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Juni asilimia za makusanyo yote zitakuwa zimefikia 100% .
Katika hatua nyingine katibu tawala Judica Omari amesema ili mafanikio haya yaendelee kuwepo ni vyema ushirikiano uliopo uendelee kudumishwa kwa ngazi zote kiutendaji ,huku akitoa wito kwa Halmashauri Nyingine za mkoa wa njombe kuja kujifunza Njombe Mji kwenye suala zima la ukusanyaji na usimamizi wa mapato ili kuweza kufanikiwa na kufikia malengo kwa pamoja.
Kwa kuzingatia ushauri na mapendekezo ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) katika kushughulikia hoja mbalimbali, kwa mwaka wa fedha 2021/2022,Halmashauri ya Mji Njombe imepata hati safi kwa hesabu kuu za halmashauri,hesabu za mradi wa mfuko wa afya wa pamoja (Health sector Busket fund) na hesabu za mradi wa mfuko wa wanawake ,vijana na watu wenye ulemavu (WYDF na PWDs) na kuiwezesha kudumu kwenye hati safi kwa kipindi cha miaka minne mfululuzo tangu mwaka 2018 hadi 2022.
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe