• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Halmashauri ya Mji Njombe yatoa Milioni 239 ya mikopo katika robo ya tatu

Tarehe iliyowekwa: April 16th, 2021

Halmashauri ya Mji Njombe imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni mia mbili thelathini na tisa  laki tisa na themanini elfu kwa vikundi 24, vikundi 08 vikiwa ni kwa   vijana na vikundi 16 vya wanawake hii ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Serikali  ambapo Halmashauri imeweza kutenga asilimia kumi za mapato yake ya ndani kwa ajili ya zoezi hilo.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya hundi ya mfano Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Romanus Mayemba ameipongeza Halmashauri kwa jinsi ambavyo imeweza kufanya usimamizi na kuhakikisha kwamba maagizo ya Serikali ya utoaji mikopo bila riba yanatekelezwa katika kila robo na kuwafikia walengwa kwa wakati.

“Niwapongeze wale wote mliobahatika kupata mikopo.Fedha za mikopo zinazotolewa zinajumuisha asilimia kumi ya mapato ya ndani pamoja na marejesho. Unaporejesha mikopo unatoa fursa kwa vikundi vingine vyenye sifa kuweza kukopa lakini pia unajijengea sifa ya kukopeshwa kwa mara nyingine. Tuzingatie urejeshaji wa mikopo kwa wakati. Tunapokwenda kutumia mikopo tuwe na uhakika wa kuirejesha na hii itatusaidia kusukuma maendeleo kwenye Halmashauri yetu. Uaminifu ni jambo la msingi sana. Alisema Mayemba

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Bi. Illuminatha Mwenda amesema kuwa Halmashauri imeweza kutoa mikopo mingi kutokana na ukusanyaji mzuri wa mapato ya ndani jambo ambalo linapelekea ongezeko la utoaji mikopo kila wakati na hivyo amewataka Wananchi kuhakikisha kuwa wanakuwa wachangiaji wazuri wa mapato na kuwa wasimamizi kwa kuhakikisha kuwa hakuna upotevu wa mapato kwani mafanikio hayo ni kutokana na makusanyo ya mapato ya ndani kuwa mazuri.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti baadhi ya  wawakilishi wa vikundi hivyo wameipongeza Halmashauri kwa jitihada hizo na wameahidi kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kufanya marejesho na kupata fursa ya kuweza kukopeshwa tena.

Kwa upande wake Donas Innocent Kayombo  mwakilishi kutoka kikundi cha Vijana Melinze  amesema kuwa changamoto kubwa wanayokabiliana nayo vijana kwenye uundaji wa vikundi ni ukosefu wa shughuli ya pamoja jambo linalopelekea vijana wengi kushindwa kujiunga kutokana na kuwa kila kijana anakuwa na shughuli yake ya kujiongezea kipato na hivyo kuiomba Serikali kuweza kuboresha miongozi hiyo ili kasi ya ukopaji kwa vijana iwe kubwa.

“Tulikuwa tunasikia mitaani kuhusu mikopo. Tukaamua kuunda kikundi. Tuliomba milioni kumi na tumepata kadri tulivyoomba na tunakwenda kuinuka kiuchumi.”Alisema Kayombo

Naye Rehema Nyezi mwakilishi kutoka kikundi cha wanawake  amesema kuwa wanaishukuru Halmashauri kwani wameweza kupatiwa mkopo kadri walivyoomba na amesema kuwa lengo lao ni kwenda kuanzisha kilimo cha parachichi na kuendeleza mradi wa ufugaji kuku na wameahidi kwenda kufanyia kazi fedha hizo ili waweze kuzirejesha kwa wakati.

Ikumbukwe kuwa kwa kipindi cha mwaka 2020/2021 Halmashauri imeweza kutoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya  shilingi  milioni mia tisa arobaini  laki nane na themanini  kwa vikundi 96 ambapo  72 vya wanawake 22 vijana na 2 walemavu ikiwa ni mapato ya ndani ya Halmashauri na fedha za marejesho. Rai imeendelea kutolewa kwa watu wenye ulemavu  kuchangamkia fursa ya ambapo kwa sasa kumekuwa na mabadiliko ya idadi ya wanaojiunga ambapo   hata mlemavu mmoja anaweza kuomba na kupatiwa mkopo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe