• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Halmashauri ya Mji Njombe Yatoa Milioni Mia Saba kwa Vikundi 72

Tarehe iliyowekwa: December 2nd, 2020

Halmashauri ya Mji Njombe imetoa kiasi cha Shilingi milioni mia saba laki tisa kwa vikundi 72 vya kiuchumi vya Wanawake, Vijana na Walemavu kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2020/2021.

Kiasi hicho cha fedha kinatokana na makusanyo ya mapato ya ndani ambapo kiasi cha Shilingi milioni 120 zimechangiwa, huku kiasi kilichosalia ikiwi ni fedha za marejesho.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi mfano wa hundi kwa vikundi hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhandisi Marwa Rubirya amevitaka vikundi hivyo kufanya matumizi sahihi ya mikopo hiyo ili kuwa endelevu na  kufanya marejesho kwa wakati jambo litakaloviwezesha vikundi vingine kukopa.

“Mikopo hii ikatumike kwa malengo yaliyokusudiwa. Sio mnatumia fedha hizi kama kikundi mkifika kule mnagawana.Mwingine anaenda kununua baiskeli mwingine anaenda kulipa ada ya shule.Hayo sio malengo ya mkopo huu.”

Awali akiwasilisha taarifa ya hali ya utoaji wa mikopo katika Halmashauri Afisa Maendeleo ya Jamii Enembora Lema amesema kuwa Hali ya utoaji wa mikopo katika Halmashauri imeendelea kuimarika kila wakati kwani kwa mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri ilitoa TSH. 375,733,00, Mwaka 2019/2020 ilitoa TSH. 676,300,000 na Mwaka 2020/2021 kwa robo ya kwanza pekee Halmashauri imeanza kwa kutoa TSH  700,900,000/=

Kwa upande wao mwakilishi kutoka kundi la walemavu na wanawake wamesema kuwa ni vyema wanavikundi kutumia fedha hizo kuchochea shughuli za maendeleo jambo litakalopelekea kufanya marejesho kwa wakati.

“Tukisema tuchepushe kidogo hii fedha marejesho yatatushinda.Tutaanza kulalamika fedha ya Halmashauri inamkosi kumbe mkosi ni sisi wenyewe.”Alisema Mwakilishi wa Wanawake.

Aggrey Chatanda ni Mwakilishi kutoka Kundi la vijana amesema kuwa fedha hizo zitakwenda kuongezea nguvu kwenye mradi wa nyuki ambao tayari umeanza.

Utaratibu wa Utoaji wa mikopo bila riba kwa vikundi vya Wanawake,Vijana na Wenye ulemavu ulianzishwa ili wanufaika waweze kupata mitaji na kufanya uwekezaji katika shughuli za kiuchumi, Mathalani katika Kilimo,Ufugaji,Uvuvi na kuanzisha viwanda vidogo vidogo na hatimaye kuweza kuboresha Maisha kuanzia ngazi ya Familia,Jamii na Taifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe