• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Halmashauri ya Mji Njombe Yatoa Mkopo wa Trekta la Milioni 75

Tarehe iliyowekwa: November 22nd, 2019

Halmashauri ya Mji Njombe imekabidhi trekta lenye thamani ya shilingi milioni 75 kwa muungano wa vikundi 5 vijulikanavyo kama Lusitu Agribusiness Group ikiwa ni mkopo utokanao na asilimia 10 za mapato ya ndani  ambapo hutumika kutoa mikopo kwa vikundi vya  vijana, wanawake na walemavu.

Akizungumza wakati wa kukabidhi trekta hilo Mbunge wa Jimbo la Njombe Kusini Edward Mwalongo amesema kuwa anaipongeza Halmashauri kwa ubunifu huo ambao utaleta chachu kwa jamii kujiunga katika vikundi na kuchochea  maendeleo katika jimbo hilo.

“Halmashauri ya Mji Njombe imewezesha wananchi kupata kitendea kazi kupitia mikopo ya asilimia kumi. Niwaombe kuwa watunzaji wa trekta hili na kuhakikisha kuwa mkopo unarejeshwa ili tuweze kukopesha na wengine. Wito wangu ni kwa wale wote waliokopeshwa fedha za asilimia kumi za mapato ya ndani kuhakikisha kuwa zinarudishwa kwa wakati ili waweze kupata fursa ya kuongezewa mikopo na kukopesha vikundi vingine” Alisema Mwalongo

Wakizungumza kwa wakati tofauti tofauti Katibu wa kikundi hicho Benson Mgaya na Mwenyekiti wa Kikundi Claudia Mhenga  wamesema kuwa trekta hilo litarahisisha uendeshaji wa shughuli za kilimo  kwa wakati kwani changamoto kubwa iliyokuwa ikiwakabili ni upatikanaji wa trekta kwa ajili ya kulima mashamba na kubeba mazao jambo ambalo awali lilikuwa linasababisha kushindwa kulima kwa kiasi kikubwa  na wakati mwingine kupelekea mazao kuoza na kuharibiwa na mvua kutokana na changamoto ya ubebaji wa mazao wakati wa uvunaji.

“Tulikuwa tukiwaza wapi tutapata mkopo wa trekta kwa ajili ya kuturahisishia shughuli zetu. Tunaishukuru Halmashauri kwamba ilikubaliana na wazo letu. Sasa tunaenda kufanya kazi. Alisema Claudia Mhenga Mwenyekiti wa Kikundi”

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Bi. Illuminatha Mwenda amesema kuwa kutokana na kuwa kikundi hicho kimeonesha nia ya dhati ya kujikwamua kiuchumi kwa kushiriki katika shughuli za uzalishaji Halmashauri imewaunga mkono kwa kuwapatia lita mia moja za mafuta ili kuweza kuanzia shughuli zao.

Katika kila robo mwaka Halmashauri ya Mji Njombe imeendelea kutekeleza maagizo ya Serikali kwa Kuhakisha kuwa asilimia kumi zitokanazo na mapato ya ndani zinatengwa kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya  wanawake, vijana na walemavu.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe