• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Halmashauri ya Mji Njombe yatoa Motisha Shule zilizofanya vizuri Mitihani ya Taifa

Tarehe iliyowekwa: June 16th, 2021

Halmashauri ya Mji Njombe imetoa kiasi cha shilingi milioni 4 kwa Shule 8, Sekondari Shule 4 na Msingi 4 ikiwa ni sehemu ya motisha kwa ufaulu mzuri katika mitihani ya Kitaifa ya kidato cha nne na cha saba ambapo kiasi cha shilingi laki tano kimetolewa kwa kila shule.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda amesema kuwa licha ya kuwa Waalimu hao wamekuwa wakisimamia taaluma katika Shule zao pia wamekuwa ni msaada mkubwa katika kusimamia maendeleo kwenye Shule hizo.

“Tumeona kazi mnayofanya ni kubwa na hatungependa kuwaacha hivi. Hii ni asante kwa kazi kubwa mnayofanya ya kusimamia taaluma kwenye maeneo yenu. Kwa bajeti ijayo tumeona tutenge fedha ili kuendelea kuleta hamasa kwa waalimu kufanya vizuri zaidi. Tunaamini kazi mnayofanya ni kubwa na sisi tupo nyuma yenu.”Alisema Mwenda

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Huduma za Jamii Halmashauri ya Mji Njombe ambaye ni Diwani wa Kata ya Luponde Ultrick Msemwa amesema kuwa mchango wa waalimu katika Halmashauri ni mkubwa kwani wanachangia katika ufaulu ndani ya Mkoa wa Njombe na pia kuipatia heshima Halmashauri.

“Tuendelee kuitetea nafasi ya kufanya vizuri na tuendelee kufanya vizuri zaidi na kupandisha ufaulu katika Shule zetu. Sisi kama wawakilishai wa Wananchi ambao watoto wetu ndio mnaowafundisha tumejitahidi kwa kadri inavyowezekana kwa chochote kilichopo ndani ya Halmashauri na ninyi muweze kupata.Niendelee kuwatia moyo na kuwaambia kuwa licha ya kuwepo na mazingira mbalimbali kwenye shule, Baraza la Madiwani na Halmashauri inaendelea kupambana siku hadi siku kuhakikisha kuwa inaboresha mazingira ya kufanyia kazi ikiwa ni ujenzi wa madarasa na ofisi  na ujenzi wa   nyumba za waalimu ili mazingira ya ufanyaji kazi yawe rafiki.”Alisema Mheshimiwa Msemwa.

Akizungumza kwa niaba ya Waalimu waliopatiwa motisha Mkuu wa Shule ya Sekondari Mpechi Brown Kiswaga amesema kuwa wanaishukuru Halmashauri kwa kujali na kuona umuhimu wa kazi wanayofanya na kusema kuwa jukumu walilonalo ni kuhakikisha kuwa mwakani wanafanya vizuri zaidi na idadi ya shule zitakazokuwa zimefanya vizuri kuwa nyingi zaidi ya sasa kwa kuendelea kuhamasishana.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe