• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Halmashauri ya Mji Njombe yawashika mkono Wazee

Tarehe iliyowekwa: July 15th, 2021

Halmashauri ya Mji Njombe imeendelea na utaratibu wa kuwapatia misaada makundi ya watu wenye mahitaji maalumu ambapo kiasi cha shilingi milioni moja laki sita kimetolewa kwa kikundi cha wazee 8 kutoka katika Kata ya Uwemba Kijiji cha Njoomlole kwa ajili ya kuwasaidi wazee hao kwenye shughuli za kujiongezea kipato na kuboresha makazi yao.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya fedha hizo Afisa Ustawi wa jamii Halmashauri ya Mji Njombe Petro Mahanza amesema kuwa Kitengo cha ustawi wa jamii kimeendelea kuwashika mkono watu wenye mahitaji mbalimbali na kuwa sauti kwa wasio na sauti wakiwemo wazee,watoto na watu wenye ulemavu.

“Kilio chenu kimesikika kulingana na mahitaji yenu. Mkurugenzi wa Halmashauri ametoa kiasi cha shilingi milioni moja laki sita na kila mzee atapata kiasi cha shilingi laki mbili.”Alisema Mahanza

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Uwemba Jactan Mtewele amekitaka kikundi hicho cha wazee kijulikanacho  kama TWITANGE MAGUFULI kuzitumia fedha hizo kulingana na mahitaji waliyoyaombea  na kuwa mfano mzuri.

“Yapo mahitaji mbalimbali ambayo wazee mliweza kuyaainisha katika andiko lenu ambalo mlinipatia.Tukumbuke kuwa andiko lenu lipo katika Ofisi yangu,Ofisi ya Afisa Maendeleo wa Kata, Ofisi ya  Mtendaji Kata  na Katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri. Wapo walioomba fedha kwa ajili ya kufuga kuku, kupanda parachichi, na shughuli mbalimbali.Itashangaza siku Mkurugenzi akitaka kuwatembelea na kuona shughili mlizofanya mara baada ya kupewa fedha na tukafika tusione kilichofanyika.Niwasihi chochote mtakachoenda kukifanya kiende sehemu sahihi”Alisema Diwani Mtewele.

Maafisa Maendeleo kutoka Halmashauri ya Mji Njombe Christina Tengay na Afisa Maendeleo Kata ya Uwemba  Flora Kapinga  wao wamesema kuwa licha ya kuwa wazee hao wamepatiwa fedha hizo wataendelea kuwasimamia ili kufanikisha shughuli zao na kuwashirikisha wataalamu wa ugani na mifugo kwa wazee waliopanga kufanya shughuli za kilimo na mifugo.

“Tunachokiomba ni utekelezaji. Sisi kama wataalamu huwa tunakwenda kuomba fedha hizi kwa Mkurugenzi inabidi mkawe chachu kwa wengine wenye mahitaji. Sisi tunatamani tuone maendeleo yanapatikana kwa sababu fedha hiyo inakidhi hitaji la kila mmoja kwa kadri alivyoiombea.”Christina alisema

Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha hizo baadhi ya wawakilishi kutoka kikundi hicho cha wazee akiwemo Illuminatha Mlowe, Mikaela Samlongo  ambaye ni Mwenyekiti wa Kikundi cha TWITANGE MAGUFULI ametoa shukrani zake kwa uongozi mzima wa Halmashauri na kuahidi kufanya kazi kwa kadri ya mahitaji yao na amewataka wazee wengine kuiga mfano huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe