• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Halmashauri ya Mji Njombe yaziburuza Halmashauri za Miji Nchini ni Mashindano ya Usafi na Mazingira. Yaibuka kidedea

Tarehe iliyowekwa: November 23rd, 2018

Halmashauri ya Mji Njombe imeshika nafasi ya kwanza kwa upande wa Halmashauri za Miji kwa kuibuka kidedea kwenye mashindano ya Usafi na Mazingira Nchini na kukabidhiwa zawadi ya trekta na tuzo maalumu huku sekondari ya wavulana Njombe ikishika nafasi ya kwanza kwa shule  za sekondari za serikali nchini na kukabidhiwa zawadi ya tuzo maalumu na pikipiki.

Hayo yamebainishwa leo wakati wa kuwakabidhi zawadi washindi wa mashindano hayo ikiwa ni sambamba na kuhitimisha kilele cha wiki ya Usafi na Mazingira Kitaifa ambapo mgeni rasmi katika Halfa hiyo alikuwa Waziri Mkuu wa Nchi Mhe. Kassim Majaliwa Kassim hafla iliyofanyika katika ukumbi wa wa Julius Nyerere- Mipango jijini Dodoma.

Akihutubia katika hafla hiyo Waziri Mkuu amewataka Wakurugenzi nchini kuhakikisha kuwa kufikia Desemba 31 kila Halmashauri iwe imefikia lengo la kuhakikisha kuwa kila familia na jamii  inakuwa na vyoo bora na vya kisasa kwani vitasaidia kupunguza uwezekano wa kutokea magonjwa ya milipuko ambayo yanaweza kusababishwa na ukosefu wa vyoo bora.

“Niwatake muhakikishe Maofisa Afya wanawezeshwa katika kutoa elimu kwa Wananchi ili suala la ujenzi wa vyoo bora na vya kisasa litekelezeke kwa ufanisi mkubwa na Maofisa afya muhakikishe mnafanya Ukaguzi wa mara kwa mara ili jambo hili liweze kufanikiwa.”alisema Waziri Mkuu.

Kwa upande wake Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema katika awamu ya pili ya Kamapeni ya Taifa ya Usafi wa Mazingira wizara yake imejipanga kuhakikisha asilimia 75 ya kaya nchini zinakuwa na vyoo bora na kuondoa kaya ambazo hazina vyoo kabisa ambapo kupitia kampeni hiyo iliyoanza imewezesha kupunguza idadi ya kaya zisizokuwa na vyoo kutoka asilimia 9.5 (2015) mpaka kufikia 3.8 (2018).

Wakizungumza mara baada ya kukabidhiwa zawadi hizo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Edwin Mwanzinga amesema kuwa ushindi huo kwa upande wa Halmashauri yake inaonesha ni kwa jinsi gani wananchi wa Mkoa wa Njombe wanakerwa na swala la uchafu wa Mazingira na amesema kuwa zawadi hizi zitaenda kuleta chachu ya utunzaji Mazingira  kwa kuhakikisha kuwa wananchi wanashiriki ipasavyo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda amesema kuwa ushindi huo ni wa halmashauri kwa ujumla kwani kila mtu amehusika kwa namna moja au nyingine katika kuhakikisha kuwa ushindi huo unapatikana na amewaomba wananchi kuendelea kuchangia tozo za taka kwa wingi kwani mafanikio sio kitu cha kiurahisi.

Mkoa wa Njombe umeweka heshima kwa upande wa Usafi na Mazingira ambapo Halmashauri ya Mji Njombe na Halmashauri ya wilaya ya  Njombe zimekuwa za kwanza Kitaifa kwa upande wa Halmashauri za Miji na wilaya,na kufanikiwa kutoa vijiji bora na shule bora ya sekondari ya serikali Njombe.

Ikumbukwe kuwa kwa awamu ya tatu mfululizo Halmashauri ya Mji na Wilaya ya Njombe zimekuwa mabingwa wa mashindano hayo na kuibuka na zawadi nono za trekta na magari ambapo rai imetolewa kwa Halmashauri nyingine kuiga mfano wa Halmashauri ya Mji Njombe na Wilaya ya Njombe.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe