• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Halmashauri yasaini mikataba na vikundi vilivyokopeshwa

Tarehe iliyowekwa: November 17th, 2021

Halmashauri ya Mji Njombe leo imesaini mikataba na vikundi vilivyopatiwa mikopo ya asilimia kumi ikiwa ni miongoni mwa hatua muhimu zilizopo kwenye miongozo ya uchukuaji wa mikopo hiyo.

Akizungumza wakati wa zoezi la utiaji saini wa mikataba hiyo Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri Enembora Lema amesema kuwa licha ya kuwa vikundi vimekuwa vikijitahidi kushiriki katika shughuli za ujasiriamali bado kumekuwa na changamoto ya vikundi vya wanawake kwani wengi wao wamekuwa wakichukua fedha na kugawana badala ya kuziingiza kwenye shughuli za ujasiriamali jambo ambalo limekuwa likipelekea kuchelewa kwa marejesho.

“Kila kikundi kina shughuli ambayo imekiwezesha kupata mkopo kwa kadri ya maombi yenu. Baada ya wiki mbili tutapita katika kila kikundi na kuhakiki shughuli ambazo mmeelekeza fedha hizo. Kwa wale ambao mnamawazo ya kwenda kugawana fedha hizo tuache mara moja” Alisema Afisa Maendeleo

Naye Afisa Maendeleo anayeshughulikia mikopo Christina Daniel amevitaka vikundi hivyo kuhakikisha kuwa wanakuwa na utunzaji sahihi wa taarifa za kikundi hususani taarifa za fedha na kuhakisha kuwa wanavikundi wanashiriki ipasavyo katika vikao vya kikundi ili kujenga uelewa wa pamoja na kujua yale yanayoendelea ndani ya kikundi husika.

“Kumekuwa na tabia ya baadhi ya wanavikundi kutohudhuria kwenye vikao hili jambo sio zuri kwani kama kikundi kuna mambo inabidi kukubaliana kwa pamoja. Wanufaika wengi wa mikopo hii ni wa Kata za Mjini inawezekana baadhi mmepanga. Inapotokea umehama toa taarifa kwa wanakikundi wengine”Alisema Christina

Katika hatua nyingine Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika akizungumza na wanufaika wa mikopo hiyo mara baada ya kuwatembelea na kushuhudia zoezi la ujazaji mikataba. Mbunge huyo amewataka wanufaika wa mikopo ya asilimia kumi kuhakikisha kuwa wanarejesha mikopo kwa wakati ili iweze kuwanufaisha na wengine.

“Njombe tumeweza kutoa bilioni kwenye mikopo.Hii inaashiria kuwa uchumi wetu umeimarika na utaratibu wa utoaji asilimia kumi unatekelezwa.Tunatoa pongezi kwa wafanyabiashara na walipa kodi wa Njombe. Wao ndio walioleta hizo fedha.Tunazidi kuiomba Serikali iendelee kuweka utaratibu mzuri zaidi ili kuweza kufikia malengo kwenye hii mikopo.Alisema Mwanyika

Aidha Mwanyika ameahidi kuvitembelea vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo na kutoa fedha kiasi cha  shilingi laki tano kwa kila kikundi kwa jumla ya vikundi vitatu vitakavyokuwa vimefanya vizuri ikiwa ni zawadi na motisha kwao kuendelea kuongeza bidii kwenye shughuli za kiuchumi.

Ikumbukwe kuwa mnamo tarehe 15 mwezi Novemba Halmashauri ilikabidhi hundi ya shilingi bilioni 1.2 kwa vikundi 116 vya vijana,wanawake na watu wenye ulemavu katika tamasha la Njombe ya Mama Samia lililoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe,ikiwa ni utekelezaji wa mwongozo wa Serikali wa kuzitaka Halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato yake kila robo kutoa mikopo iiyo na riba kwa vmakundi hayo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe