• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Hatuwezi kuwa Manispaa mandhari ya Mji ikiwa chafu.Madiwani Mji Njombe wazungumza

Tarehe iliyowekwa: April 29th, 2021

Wakizungumza katika Mkutano wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani wakati wa kujadili taarifa ya Kamati Mipangomiji na Mazingira Madiwani Halmashauri ya Mji Njombe wameipongeza kamati hiyo kwa hatua waliochukua ya kutekeleza maagizo ya baraza lililopita kwa kuwatoa wafanyabiashara katika maeneo yasiyo rasmi ikiwemo pembezoni mwa barabara na kutokufurahishwa na hatua iliyochukuliwa na Mkuu wa Wilaya  ya kuwarejesha tena wafanyabiashara katika maeneo hayo licha ya vikao na matangazo kutolewa ya kuwaelekeza maeneo ya kufanyia biashara na kusababisha kukinzana kwa majukumu

Wakioneshwa kutoridhishwa kwa maamuzi yaliyofanywa baadhi ya Madiwani Filoteus Mligo Diwani wa Kata ya Lugenge ,Ultrick Msemwa  Diwani wa Kata ya Luponde na Nestory Mahenge Diwani wa Kata ya Mji Mwema  wamesema kuwa Halmashauri ya Mji Njombe ipo katika hatua za awali za kupeleka mapendekezo ya kuipandisha hadhi Halmashauri na hivyo  uwepo wa Wafanyabishara barabarani ni mojawapo ya vikwazo vitakavyopelekea kushindwa kufikia malengo hayo.

Madiwani hao kwa pamoja waliafiki maeneo ambayo si rasmi kutokuendelea kutumika kwa ajili ya kufanyia biashara hizo na wamewataka Watumishi kuendelea kusimamia zoezi la usafi na kumwomba Mkuu wa Wilaya kuchukua hatua za haraka ili kuweza kunusuru Mji wa Njombe na hali ya uchafu iliyopo sasa na ongezeko la wafanyabiashara barabarani.

“Hatuwezi kuwa na Mji wa kuuza mali mbichi kila mahali.Serikali imewekeza fedha nyingi kwenye ujenzi wa soko.Lakini wafanyabishara waliopo sokoni nao wanatoa malimbichi na kuuza nje ikiwemo barabarani.Inabidi  tusimamie ipasavyo usafi wa mji na kutowaendekeza wale wote wanaokiuka kanuni za usafi wa mazingira.”Alisema Diwani

Awali Akiwasilisha salamu za Serikali Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi. Ruth Msafiri amewataka Waheshimiwa Madiwani kufanya kazi kwa bidii na kwa malengo na kuhakikisha kuwa usimamizi wa miradi unafanyika kwa ufanisi mkubwa ili adhma ya Serikali iweze kutimia.

Aidha Mkuu wa Wilaya amesema kuwa licha ya uwepo wa Maagizo mbalimbali yanayotolewa katika vikao mbalimbali ni vyema utekelezaji wa maagizo hayo ukafanywa kwa kuzingatia sheria,kanuni na taratibu na bila uonevu ili haki iweze kutendeka kwa kila Mwananchi.

Agenda nyinginge iliyoweza kuzua mjadala ni pamoja na uwepo wa shule kwa ajili ya watoto wenye vipaji ya Utalingolo hoja iliyoibuliwa na Diwani wa Kata ya Matola Edwin Mwanzinga ambapo kwa amesema kuwa uwepo wa shule hiyo utasababisha kushuka kwa ufaulu kwani watoto wenye ufaulu wa juu wanatakiwa kuchanganyika na wenye ufaulu wa kati na wa wastani ili kuweka mchanganyiko mzuri katika kujifunza na kuomba Idara ya elimu kuwapeleka wanafunzi kulingana na ufaulu wao.

“Mimi sikubaliani na uwepo wa shule ya watoto wenye vipaji maalumu.Katika Kata yangu wale wote wenye ufaulu wa A mmewachukua tumebaki na wenye ufaulu wa B na C.Mazingira ndio hupelekea wakati mwingine mtoto kushindwa kufanya vizuri. Mimi nakubaliana na ubadilishanaji wa Wanafunzi. Wanafunzi wa Matola wasome Utalingolo na Utalingolo au Kata nyingine wasome Matola. Lakini utaratibu wa ufaulu wa A wawe na shule yao maalumu huo utasababisha Halmashauri yetu ishindwe kufanya vizuri kwani watoto hao wanatakiwa kuchangayika ili wale wenye ufaulu mdogo waweze kujifunza kwa wenzao wenye ufaulu mkubwa. Alisema Mwanzinga

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri  Erasto Mpete ambaye ni Diwani wa Kata ya Utalingolo amesema kuwa lengo la uanzishaji wa shule hiyo ni kuleta hamasa na ushindani kwa wanafunzi ambao wanataraji kuingia kidato cha kwanza ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao lakini si kushusha ubora wa elimu.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Halmashauri Romanus Mayemba ameipongeza Halmashauri kwa kuendelea kusimamia mapato ambapo kufikia mwezi machi Halmashauri imeweza kukusanya mapato kwa asilimia 96.3 ya lengo na hivyo kuhimiza usimamizi zaidi ili lengo liweze kutimia huku ikiwa imesalia miezi miwili kufunga mwaka wa fedha.

Halmashauri ya Mji Njombe ipo katika hatua za awali za kufanikisha vigezo vitakavyoiwezesha Halmashauri hiyo kupanda hadhi kutoka kuwa Mji na kuwa Manispaa huku changamoto kubwa ikiwa ni uwepo wa Wafanyabiashara wanaofanya biashara katika maeneo ambayo si rasmi jambo linaloharibu mandhari ya Mji na kuifanya Halmashauri kushindwa kukidhi vigezo katika mashindano ya usafi na mazingira na hivyo kupoteza sifa yake ya usafi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe