• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Idara ya Afya Yawapiga Msasa Wafanyabiashara

Tarehe iliyowekwa: May 22nd, 2019

Idara ya Afya Halmashauri ya Mji Njombe kupitia mratibu wa TFDA wa Halmashauri wametoa mafunzo kwa Watendaji wa Mitaa na wafanyabiashara wa chakula na vipodozi  lengo ikiwa ni kuwajengea uwezo kuhusu sheria  zinazosimamia masuala ya chakula, dawa na vipodozi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mafunzo hayo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Njombe  Dkt. Thomas  Samwel Ndalio amesema kuwa mafunzo hayo yanalenga  kuelezea  taratibu sheria  na kanuni za Mamlaka ya Chakula na Dawa  tozo zinazotumika, haki na wajibu wao katika kuhakikisha kuwa utekelezaji wa sheria za mamlaka ya chakula dawa na vipodozi zinatekelezwa ipasavyo.

“Kumekuwa na changamoto wakati wa kusimamia sheria hizi za TFDA. Changamoto hii ni kwa wale waliokasimiwa madaraka ya kusimamia sheria (Halmashauri) pamoja na Wafanyabishara. Wafanyabiashara wengi hawaelewi tozo wanazotozwa wanatozwa  kwa mujibu wa sheria zipi na ndio maana leo tumeamua tuwapatie elimu ili wawe na uelewa wa pamoja lakini pia tunaamini watakuwa waalimu bora kwa wafanyabiashara wengine.”Alisema Ndalio

Akizungumzia manufaa ya mafunzo hayo Mtendaji wa Mtaa wa Mpeto Agnes Flowin Mbilinyi alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwao na yanafaa kuwa endelevu.

“Nimejifunza vitu vingi sana hususani kwa wafanyabiashara wanaofanya biashara za vyakula, dawa na vipodozi. Kwa sasa itakuwa rahisi kufanya kazi ya ukaguzi kwani tayari nimetambua wajibu wangu katika kusimamia sheria za Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi ninawaomba wafanyabishara  kuhakikisha kuwa wanafuata sheria ipasavyo ili kuepuka  kuchukuliwa hatua pindi wanapokwenda kinyume na sheria.”Alisema Mtendaji huyo.

Kwa upande wake mmoja wa washiriki katika mafunzo hayo Happines Chengula ambaye ni Mfanyabiashara wa bidhaa za vyakula  Katika Kata ya Mjimwema alisema kuwa  mafunzo hayo yamemjengea uwezo wa kuhakikisha kuwa bidhaa zake zinakuwa na nembo ya ubora TBS na zimethibitishwa na Mamlaka ya chakula na dawa TFDA Ili kulinda afya ya mlaji.

Julius Kahogo ambaye ni mfanyabiashara  wa bidhaa za vyakula na vipodozi Mjini Njombe alisema kuwa watendaji wamepewa majukumu ya kusimamia sheria lakini ni vyema busara kutumika na kuhakikisha elimu inatolewa zaidi.

 “Zipo kaguzi ambazo huwa zinafanyika lakini Watendaji wamekuwa hawafanyi ipasavyo. Watendaji wengi wamekuwa wakifanya ukaguzi kwa lengo la kukusanya mapato lakini sio kutoa elimu. Wakati mwingine sio kila mtu anakuwa na ufahamu wa jambo ni vyema ukamuelimisha mtu kwanza. Leo kila mtu amepata elimu na mipaka ya kazi kati ya watendaji na wafanyabiashara imeelezwa vizuri.”Alisema 

Wafanyabiashara hao wameiomba Halmashauri kupitia Mratibu wa TFDA kuhakikisha kuwa mafunzo hayo yanakuwa endelevu na kuhakikisha kuwa taarifa inafikia wafanyabiashara wengi zaidi ili kwa kipindi kingine waweze kuhudhuria kwa wingi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe