• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

IFAD YAPONGEZA MAANDALIZI YA MRADI WA MAGEUZI YA TASNIA YA MAZIWA.

Tarehe iliyowekwa: August 15th, 2025

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo (IFAD) nchini Tanzania, akiambatana na Msajili wa Bodi ya Maziwa, Prof. Msalya, pamoja na Mratibu wa Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa kwa kuzingatia Mabadiliko ya Tabianchi, amefanya ziara katika Halmashauri ya Mji Njombe kufuatilia maandalizi ya utekelezaji wa mradi huo. 

Ziara hiyo ilianza kwa kutembelea Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe, kisha Kiwanda cha Kusindika Maziwa cha Kends Milk Factory kilichopo Mtaa wa Ngalanga. Hatua ya mwisho, tarehe 15 Agosti 2025, ilikuwa kukutana na wafugaji wa Kijiji cha Igominyi, hususan kikundi cha Muungano, ambacho kimenufaika na mpango wa “Kopa Ng’ombe, Lipa Ng’ombe wa Maziwa” unaolenga kusaidia kaya maskini. 

Mkurugenzi wa IFAD alieleza kuridhishwa na juhudi za Halmashauri ya Mji Njombe katika kuwezesha jamii, akisisitiza kuwa mradi huo utaleta mageuzi chanya kwenye sekta ya maziwa na kuongeza kipato cha wananchi. Aidha, alifurahishwa na mapokezi kutoka kwa wafugaji na kuahidi kutoa fedha kusaidia utekelezaji wa mradi huo. 

Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa kwa kuzingatia Mabadiliko ya Tabianchi (Climate Smart Dairy Transformation Project – C-SDTP) unafadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo IFAD, OPEC, French Development Agency, Green Climate Fund, Heifer International na BEN.

Lengo kuu la mradi ni kuboresha njia za kujikimu kimaisha, kuinua hali ya lishe katika kata masikini za wafugaji, na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi kwa wafugaji maskini. 

Mradi huu utatekelezwa kwa kipindi cha miaka 10 katika Halmashauri 22 zilizopo kwenye Mikoa 8 ya ushoroha wa uzalishaji wa maziwa Tanzania Bara na Mikoa 5 ya Tanzania Visiwani. Thamani ya mradi ni Dola za Marekani 18,783,840 (sawa na TZS 47,282,728,240). 

Katika Mkoa wa Njombe, utekelezaji utafanyika katika Halmashauri ya Mji Njombe, Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

#maendeleokwawote


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29,2025

    October 15, 2025
  • MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA YASISITIZWA KWA WAKULIMA WA MTAA WA MPOBOTA - MJIMWEMA .

    October 11, 2025
  • MWEKEZAJI MADEBE AKABIDHIWA HATI MILIKI 16

    October 11, 2025
  • WANANCHI MPOBOTA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025

    October 11, 2025
  • Angalia zote

Video

IFAHAMU HUDUMA YA KIPEKEE INAYOPATIKANA NDANI YA SOKO KUU NJOMBE.
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe