• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

JICHO LA SERIKALI LIPO KWENYE KILIMO

Tarehe iliyowekwa: January 15th, 2024

Timu ya wanafunzi na wakufunzi kutoka chuo cha Ulinzi wa Taifa (NDC) Dar es salaam,inayofanya ziara Mkoani Njombe ,imetembelea kitalu cha uzalishaji wa miche ya parachichi cha NEMES Green Garden kinachomilikiwa na mkulima Steven Mlimbila kilichopo Halmashauri ya Mji Njombe ,Mtaa wa Maheve  kata ya Ramadhani. 


Akizungumza baada kupokea taarifa ya mkulima huyo ,kiongozi wa msafara ambaye pia ni mkufunzi kwenye chuo hicho Brigedia Jenerali Erick Mhoro amesema wamefika Njombe kuona utekelezaji wa sera za Serikali kwenye sekta mbalimbali ikiwemo kilimo. 


"Tumefika hapa tuone uzalishaji wa parachichi kunzia shambani na tunashukuru tumeona uzalishaji wa miche na parachichi, kilimo hiki kwa Njombe wamepiga hatua, hongera na niseme Mlimbila ni kijana wakuigwa" Alisema Jenerali E. Mhoro. 


Amepongeza mzalishaji wa miche NEMES kwa kazi anayoifanya ambayo inonekana wazi kuwa na mchango kwenye pato la taifa kwani parachichi kutoka Njombe imejizolea sifa kwenye soko la kimataifa. 


"Kazi ni nzuri na nimependa siyo mchoyo anawafundisha na wengine. Ni jambo jema kama tulivyoeleza watu wanakuja kujifunza hapa wakawe wazalishaji kama yeye au wakubwa zaidi" Aliongeza Brigedia Jenerali E. Mhoro. 


Katika hatua nyingine amemhakikishia mkulima huyo kuwa jicho la Serikali lipo kwenye kilimo hivyo changamoto ambazo amezianisha zinafanyiwa kazi ikiwemo changamoto ya   umeme wa uhakika ambayo itakuwa historia nchini Tanzania baada yakukamilika kwa bwawa kubwa la kuzalisha umeme la Mwalimu Nyerere .


Kwa upande wake Kanali Maiyo mwanafunzi kutoka nchini Kenya, amesema anachokifanya NEMES ni cha kuigwa na vijana ambao wanapitia changamoto ya kukosa ajira kwenye nchi nyingi duniani 


Ametoa wito kwa wananchi Mkoani Njombe  haswa Vijana kuendelea kujihusisha na shughuli za kilimo hasa kilimo cha parachichi na miti kwa ajili ya mbao kwani wafanyabiashara wengi kutoka nchini Kenya hununua mbao na parachichi zinazozalishwa Njombe. 


Steven Mlimbilia ( NEMES) ni miongoni mwa wakulima wakubwa wa Prachichi Mkoani Njombe alieamua kujikitika kwenye kilimo hicho tangu mwaka 2010 na mpaka sasa anamiliki hekari 180. 


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe