• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Jitihada kumkomboa Mama na Mtoto Kituo cha Afya Kifanya zaanza.Mbunge akabidhi gari ya Wagonjwa

Tarehe iliyowekwa: June 12th, 2021

Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika leo amekabidhi gari ya kubebea wagonjwa yenye thamani ya shilingi milioni 200 katika kituo kipya cha Afya Kifanya, vyanzo vikuu vya ujenzi wa kituo hicho ikiwa ni mapato ya ndani ya Halmashauri na Nguvu za Wananchi ambapo Wananchi wa Kata ya Kifanya walichangia kiasi cha Shilingi millioni thelathini na nane na laki saba na  Halmashauri kupitia mapato ya ndani  iliweza kutoa kiasi cha shilingi milioni mia tatu hamsini.

Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa Kituo hicho Mtendaji wa Kijiji cha Kifanya Barick Kabelege amesema kuwa lengo la ujenzi wa Kituo hicho linatokana na utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuhakikisha kuwa katika kila Kata inatakiwa kuwa na Kituo cha Afya na dhumuni  la pili ikiwa ni kutokana na ongezeko la idadi ya watu wanaohitaji huduma za Kiafya katika Zahanati ya sasa ya Muungano ongezeko lililosababishwa na uwepo wa shamba la chai Mahoro na Unilever, shughuli za kibiashara na umbali wa takribani Kilomita 60 kutoka ilipo Hospitali ya Mji Kibena.

“Mpaka sasa tumefanikiwa kujenga majengo 6 ya kiwemo jengo la upasuaji, mortuary, jengo la kufulia jengo la mama na mtoto, maabara na miozi. Tunao pia wachangiaji mbalimbali ambao wamechangia katika kufanikisha ujenzi huu Hayati Dkt. John Pombe Magufuli alituchangia milioni 10, Mbunge aliyepita alichangia mifuko 100 ya saruji, Mheshimiwa Diwani mifuko 50 ya saruji, Umoja wa Wanawake CCM Wilaya ya Njombe mifuko ya saruji 20, Taasisi ta Kifedha Kifanya  kiasi cha shilingi laki saba  na nusu na CCM Wilaya mifuko 10 ya saruji ambapo kwa pamoja tumekamilisha majengo hayo.”

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano  hayo Mbunge wa Jimbo hilo Deo Mwanyika amewashukuru Wananchi wa Kifanya kwa kuitikia wito wa Serikali na kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuimarisha Sekta ya Afya katika jimbo hilo jambo lililopelekea Halmashauri hiyo kuwa kati ya Halmasahuri 20 pekee zilizofanikiwa kupata magari hayo nchi nzima.

“Ombi lenu limekua ndio msingi wa ushindi wetu.Ujenzi wa kituo cha afya kifanya ni jambo la kutukuka.Naomba niwahakikishieni kuwa mchango wangu ni kuhakikisha kuwa kituo hiki kinafunguliwa na vifaa tiba vinapatikana. Kwa leo nitawachangia mifuko 100 ya saruji ila yaliyosalia nitakwenda kuyatekelza kwa nguvu zote.Tunamshukuru pia Rais wetu Samia Suluhu Hassani kwani kwa uongozi wake Njombe tutafanya makubwa”Alisema Mwanyika

Aliendelea kusema.”Niwaombe twende tukalitunze gari hili na pia tuhakikishe kuwa tunaitambua na kuilinda mipaka ya kituo chetu ili kuepusha migogoro”Alisema

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Njombe Edward Mgaya amewapongeza Wananchi hao na kuwataka kuendeleza utamaduni wa kuchangia kwani licha ya kupatiwa gari lakini kuna wakati mwingine magari hayo yanashindwa kutoa huduma kutokana na kukosekana kwa fedha za mafuta na matengenezo na kuwataka Wabnanchi kuendelea kulihudumia gari hilo ili Wananchi waendelee kupata huduma za msingi

Atilio  Mwapinga na Leah Mkalawa wote wakazi wa Kifanya wanasema kuwa wanaishukuru Serikali kwa kupatia gari hilo kwani kwa sasa walikua wanategemea gari kutoka kituo cha afya mjini takribani kilomita 60 kama akitokea mgonjwa wa rufaa jambo ambalo lilikuwa lilikua linahatarisha maisha ya watu hususani wanawake wajawazito.

Mpaka sasa kituo hicho kipo katika hatua za umaliziaji huku kiasi cha Shilingi milioni mia mbili ishirini na tano kikitarajiwa kutumika kukamilisha ujenzi huo ambapo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminatha Mwenda amewahakikishia Wananchi kukamilisha hatua hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. June 17, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SALAMU ZA SHUKRANI

    July 01, 2025
  • SIKU NNE ZA KUSIKILIZA KERO NA MAONI YA WANANCHI LIMEHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.

    June 30, 2025
  • Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe atoa wito kwa Wananchi kujitokeza kupata huduma Stendi ya Zamani.

    June 27, 2025
  • HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAPONGEZWA KWA HATI SAFI

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video

LUNYANYWI FISH FARM YASHUGHULIKIA KERO ZA WAFUGAJI WA SAMAKI NJOMBE TC
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe