• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

JUWAKITA NJOMBE YAADHIMISHA SIKU YA MAMA KWA KUPANDA MITI.

Tarehe iliyowekwa: January 12th, 2024

Kuelekea  siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa  Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Samia Suluh Hassan, Januari 12,2024 Jumuiya ya Wanawake wa Kiislamu Tanzania (JUWAKITA) Mkoa wa Njombe kwa kushirikina na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe, imepanda miti ya mapambo zaidi ya 200 kandokando ya  barabara inayoelekea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Njombe.


Katibu wa JUWAKITA Mkoa wa Njombe Bi. Halima Hamza, amesema wametenga siku hii maalumu kwa  kupanda miti ili kumtakia Kheri ya siku ya kuzaliwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluh Hassan, ambaye alizaliwa Januari 27,1960.


Pia ametoa shukrani kwa  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa jitihada mbalimbali inazofanya katika uhifadhi wa Mazingira na uwezeshaji wa wanawake kiuchumi. 


Aidha ameeleza kuwa zoezi la upandaji miti kwa Jumuiya hiyo litakuwa endelevu na wataendelea kuhamasisha wanawake wengine na jamii kwa ujumla kupanda miti hasa wakati huu wa mvua. 


Kwa upande wake Katibu wa JUWAKITA Wilaya  ya Njombe Zaituni Mahimbo, amesema miti  waliyoipanda ni sadaka na ni alama ya kumbukumbu kwa wanafunzi walioshiriki kupanda miti hiyo na vizazi vijavyo vitakavyoishi Mkoani Njombe. 


Naye Afisa Maliasili wa Halmashauri ya Mji Njombe John Sanga ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Njombe kwenye tukio hilo, amewapongeza wanawake wa Jumuiya hiyo Mkoani Njombe kwa kuamua kuadhimisha siku ya kuzaliwa ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluh Hassan kwa kupanda miti ambayo ni kumbukumbu ya kudumu. 


Sanga amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhamashisha zoezi la upandaji wa miti na kwa mwaka huu Halmashauri ya Mji kwa kushirikina na wadau imezalisha miche  ya miti aina tofauti milioni 13 ambayo itapandwa kwenye maeneo tofauti tofauti ndani ya Halmashauri. 


Aidha ametoa wito kwa jamii kuendelea kutunza mazingira kwa kupanda miti na kuacha kuchoma misitu na kukata miti kwenye vyanzo vya Maji.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe