• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

KAMAKA Kuanza kuhakiki Vikundi vya wakopaji kuepuka hoja

Tarehe iliyowekwa: June 18th, 2021

Ni mapendekezo yaliyotolewa katika Baraza Maalumu la kujadili hoja za mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu za Serikali CAG katika Halmashauri ya Mji Njombe ambapo kwa mwaka 2019/2020 kiasi cha Shilingi Milioni 42.8 kinadaiwa kutoka kwenye madeni ya vikundi vya Wanawake na Vijana ambapo Madiwani wameitaka Kamati ya Maendeleo ya Kata (KAMAKA) kushiriki katika kuhakiki vikundi vitakavyopatiwa mikopo ili kujiridhisha.

Akichangia mapendekezo yaliyotolewa na Kamati ya fedha baadhi ya Waheshimiwa Madiwani Edwin Mwanzinga Diwani wa Kata ya Matola,Filoteus Mligo  Diwani wa Kata ya Lugenge na Diwani Viti Maalumu Njombe Mjini Tumaini Mtewa wamesema kuwa ni vyema vikundi hivyo vikaendelea kufuatiliwa kwa karibu zaidi ili wakopaji waweze kurejesha fedha hizo na hoja  ziweze kufungwa kwa wakati na pia utaratibu wa Kuwahusisha Kamati ya Maendeleo ya Kata ukafuatwa ili ufuatiliaji uwe wa ukaribu.

“Kwenye utoaji Mikopo usipotoa mikopo ni hoja. Ukitoa mikopo wasiporejesha ni hoja. Napendekeza majina ya vikundi yapitishwe kwenye KAMAKA ili tuweze kujua ni vikundi gani vinavyokopa kwenye Kata hata ufuatiliaji utakuwa rahisi. Kwenye kurejesha pia tutakamatana Madiwani humu ndani kwani sisi ndio Wenyeviti wa KAMAKA. Hii itasaidia katika kufanya marejesho kwa wakati kwa vikundi” Alisema Mwanzinga Diwani wa Kata ya Matola.

“Ukiangalia katika vikundi vinavyodaiwa wengi wanatoka katika Kata za Njombe Mjini,Ramadhani na Mjimwema. Maeneo ya Mjini wamekuwa wasumbufu katika urejeshaji wa mikopo.Ni vyema sasa katika vipindi vijavyo fedha hizi tukatoa kwa Kata zinazorejesha “Alisema Diwani wa Kata ya Makowo Honolatus Mgaya.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhandisi Marwa Rubirya ametoa muda wa miezi mitatu kuhakikisha kuwa kiasi cha Shilingi milioni 42.8 za marejesho ya vikundi zinarejeshwa ili ziweze kuwanufaisha walengwa katika maeneo mengine na ametoa miezi mingine mitatu kuhakikisha kuwa makusanyo ya shilingi milioni 61.3 ya waliokuwa mawakala wa ukusanyaji mapato ya Halmashauri yanarejeshwa kwa Halmashauri

“Tunaovijana waliomaliza mafunzo ya jeshi la kujenga taifa. Wengi hawajafanikiwa kupata ajira zilizo rasmi na wanataaluma mbalimbali. Tunaweza kuwaweka kwenye vikundi kwa kadri ya taaluma zao na kuwapatia mikopo ambayo itawasaidi katika kupata ajira stahiki” Alisema Rubirya.

Licha ya kuipongeza Halmashauri kwa ushirikiano kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kupata hati safi pia ameitaka Halmashauri kuendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato na kuendelea kusimamia utoaji wa huduma na kuipongeza kwa hatua ambayo Halmashauri imeanza kuchukua ya kuipandisha hadhi kutoka kuwa Mji kwenda kwenye Manispaa.

Kwa mwaka 2019/2020 katika miamala ya hesabu za mwisho Halmasahuri ilipata hati inayoridhisasha (Safi) ambapo Halmashauri ilikuwa na jumla ya hoja 38 kati ya hizo 19 zikiwa ni hoja za nyuma na 19 zikiwa ni hoja za mwaka husika.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe