Kamati ya fedha na Utawala Halmashauri ya Mji Njombe ikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Mhe Erasto Mpete ,Oktoba 18,2023 imefanya ziara yakutembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa Halmashauri ya Mji Njombe.
Wajumbe wa kamati hiyo wamepongeza ofisi ya mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe kwa usimamizi mzuri wa fedha za maendeleo zinazotolewa na serikali
“Nimpongeze mkurugenzi pamoja na wataalamu wote kwa kuhakikisha mnasimamia vizuri miradi inayotekelezwa kwa fedha za serikali ,tuendelee kuunga mkono jitihada za Mhe.Rais katika kuwaletea wananchi maendeleo”Alisema Mhe Mpete.
Aidha Mhe Mpete amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa namna kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Mji Njombe.
Amemshukuru Mhe Rais kwa niaba ya wajumbe wa kamati ya fedha na utawala pamoja na madiwani wote wa Halmashauri ya Mji Njombe baada yakujionea kazi nzuri ambayo imefanywa na fedha za serikali kwenye miradi ya maendeleo.
Katika ziara hiyo wajumbe wa Kamati ya fedha na Utawala walitembelea mradi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari kata ya makowo(SEQUIP),Ujenzi wa kituo cha afya kata ya luponde,Ujenzi wa madarasa 5,mabweni 3 na vyoo shule ya sekondari Yakobi pamoja na kutembelea kituo cha afya kata ya Mjimwema.
Ikumbukwe kuwa kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya Mji Njombe ilipokea fedha kutoka Serikali kuu kwa ajili utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye sekta ya elimu na afya shilingi bilioni 2,078,909,081.01
#Njombetchatukwami
#tunakwendanakasiyamama
#kazizinaendeleanakukamilika
Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.
Sanduku la Posta: S.L.P 577
Simu ya Mezani: 026-2968833
Simu ya Mkononi: 026-2968833
Barua Pepe: td@njombetc.go.tz
Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe