• Malalamiko |
    • Barua Pepe |
Njombe Town Council
Njombe Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Miundombinu na uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Mazingira na Usafishaji
      • Ununuzi
      • TEHAMA na Takwimu.
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Election
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Mawasiliano Serikalini
      • Utamaduni,Sanaa na Michezo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Sekta ya Madini
    • Kilimo na Mifugo
    • Vivutio vya utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Kilimo na Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Afya,Elimu na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Vikao vya Kisheria
      • Vikao vya Madiwani
      • Ratiba ya kumuona Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu za Maombi mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Jarida

Kamati ya Siasa CCM Mkoa wa Njombe yapongeza utekelezaji Ilani katika Halmashauri ya Mji Njombe

Tarehe iliyowekwa: August 18th, 2021

Ni katika ziara ya Kamati ya siasa CCM Mkoa wa Njombe ikiongozwa na Mwenyekiti wake Jassel Mwalala ambapo ilitembe katika mradi wa ujenzi wa shule mpya ya magufuli na jengo la upasuaji katika hospitali ya kibena lengo ikiwa ni kuangali uteklezaji wa ilani ya CCM.

Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa shule ya msingi Mratibu elimu Kata ya Ramadhan Fortunatus Mbilo amesema kuwa ujenzi huo ulifuatiwa maombi ya wanafunzi wa shule ya msingi ramadhan kwa hayati dkt john pombe mqagufuli katika ziara yake mkoani njombe ambapo wanafunzi hao waliomba bwalo la chakula na kuongezewa vyumba vya madarasa  kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi iliyokuwepo katika shule ya Msingi Ramadhan ambapo Hayati Dkt Magufuli aliwajengea bwalo na vyumba vya madarasa na ndipo wananchi walipohamasika na kuendeleza ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na baadaye halmashauri kupitia mapato ya ndani ilisaidia kuendeleza ujenzi wa madarasa 6 ofisi na vyoo.

“Wananchi wa Mtaa wa Ramadhan waliunga mkono kwa ujenzi wa madarasa matatu ofisi moja na matundu 9 ya vyoo vya wavulana kwa gharama ya Shilingi milioni 35,248,400 ambapo Halmashauri ya Mji Njombe  ilitoa kiasi cha Shilingi milioni 116,600,000 ambapo iliwezesha ujenzi wa madarasa 6 matundu 4 ya vyoo vya Waalimu,madawati 250 na matundu 11 ya vyoo vya kike.”

Wakizungumza mara baada ya kupokea taarifa hiyo na kukagua ujenzi huo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Njombe Jassel Mwalala ameipongeza Halmashauri kwa ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Magufuli na ameishauri Halmashauri kuhakikisha kuwa inaanza michakato ya ujenzi wa nyumba za Watumishi katika shule hiyo.

“Niwapongeze kwa kazi nzuri mliyoifanya kazi inavutia. Kwenye taarifa yenu nimeona kuna vyumba vimekamilika lakini havina madawati na kuna maeneo kuna madawati.Hivyo Mkurugenzi inabidi uandike kutoa maelekezo ya fedha  kuelezea kuwa tumefanya mabadiliko kwenye mradi. Hatuwezi kuwa na madarasa yamekamilika na madawati yapo huko inabidi tufanye hivi ili watoto wetu waendelee kusoma.”Alisema Mwalala

Naye Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhandisi Marwa Rubirya ameelekeza katika kila mradi kuhakikisha kuwa kunakuwepo na taarifa ya mchanganuo wa fedha kwa kila chanzo na jinsi zilivyotumika ili kuweka uwazi zaidi kwenye utekelezaji wa miradi hiyo.

Aidha katika Hatua nyingine Kamati ya CCM Mkoa wa Njombe ilifika katika Hospitali ya Kibena ambapo imefanikiwa kufika katika jengo la upasuaji katika hospitali hiyo ambalo jengo hilo limeanza kutumika na kuipongeza Unicef kwa kufanikisha ujenzi wa jengo hilo kwa kushirikiana na Halmashauri nna Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambapo mpaka sasa jumla ya wakinamamam waliofanyiwa upasuji toka kuanza kutumika ni wanawake 12.

Katika hatua nyingine Mwalala ameupongeza uongozi wa Hospitali ya Mji Kibena kwa jinsi walivyojipanga kwenye utoaji wa huduma bora na jinsi walivyoweza kuboresha mazingira ya Hospitali hiyo ambao ni kongwe.

Kamati ya Siasa CCM Mkoa wa Njombe ipo katika ziara ya kukagua na kujionea utekelezaji wa Ilani ya CCM unavyofanyika katika Mkoa huo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI,UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI. April 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA. December 20, 2024
  • MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022 May 19, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA. April 18, 2024
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKUU WA WILAYA NJOMBE MHE. JUMA SWEDA ATOA WITO KUHUSU CHANJO YA PILI YA POLIO.

    April 29, 2025
  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA NJOMBE MJINI AKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

    April 24, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA NJOMBE KUKAGUA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    April 04, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Njombe awaonya wenyeviti kuhusu uharibifu wa miradi ya maendeleo

    February 15, 2025
  • Angalia zote

Video

WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA KUJITUMA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Huduma za Afya
  • Huduma za Elimu
  • Huduma za Biashara

Kurasa Mashuhuri

  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Tovuti ya Mkoa wa Njombe
  • Watumishi portal
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha 5 na vyuo

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi yetu inapatikana barabara ya Njombe-Songea mtaa wa Mjimwema.

    Sanduku la Posta: S.L.P 577

    Simu ya Mezani: 026-2968833

    Simu ya Mkononi: 026-2968833

    Barua Pepe: td@njombetc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2017 Halmashauri ya Mji Njombe